Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwataka vijana kuwa mfano wa kuigwa
Dodoma na nchi nzima katika kampeni yao ya kujiajiri wenyewe.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwasha mtambo wa kufyatulia matofali.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akishiriki kufyatua matofali katika mtambo huo.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akizungumza na Wanafunzi waliokuwa
wanafundishwa masomo ya ziada(tution) katika ofisi ya DOYODO.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na vijana
wa taasisi ya DOYODO na Afisa Vijana kutoka Manispaa ya Dodoma alipokuwa
anakagua miradi mbalimbali mapema leo ofisini kwao mjini Dodoma.
………………………………………………………………………………..
Naibu Waziri wa Nchi ,Ofisi
ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)Mhe.Selemani
Jafo amewataka vijana wa Taasisi ya Maendeleo ya Vijana Dodoma(DOYODO)
kuongeza ubunifu ili waweze kuwa washindani katika soko la biashara kwa
kutumia fursa ya wahamiaji wanaokuja Dodoma.
Mhe.Jafo aliyazungumza hayo
alipokuwa anakagua miradi mbalimbali ya taasisi hiyo mapema leo na
kuwataka kuwekeza kwenye kilimo kwa kuwa wanafikilia kupata eneo lao
wenyenye ni vyema kupata hekari moja kwa ajili ya kilimo cha mboga
mboga na matunda kwani kinalipa.
’’Kumekuwa na tabia ya vijana
kuchagua kazi na baadhi yao kusubiri kupata ajira kutoka Serikalini
lakini nyie mmetoa mfano badala ya kutegemea ajira, mmejiajiri na
ntahakikisha baadhi ya wabunge wanakuwa wa kwanza kuja kununua matofali
hasa kwa wale wanaojenga Dodoma ’’
“Nitaongea na Mkurugenzi wa
Manispaa ya Dodoma ili mpatiwe milioni moja kutoka mfuko wa 5%ya
makusanyo ya Manispaa ya Mapato ya vijana na milioni kumi kutoka Ofisi
ya Waziri Mkuu na mimi nachangia kwa kununua matofali mia tano
“Mhe.Jafo aliahidi.
Naye Afisa Mipango na Muhasibu wa
DOYODO Elias Mbogo amesema taasisi inajipatia kipato chake kupitia
vyanzo mbalimbali ikiwemo ada ya uanachama,tozo,miradi yao na misaada
kutoka kwa wadau wa Taasisi.
Taasisi ya DOYODO imesajiliwa
kisheria mwaka 2002 na kuanza kufanya shughuli zake rasmi toka 2015 na
miradi waliyonayo ni mradi wa matofali,tuition(elimu),ufundi chelehani
na kukodisha ukumbi kwa ajili ya semina na sherehe mbalimbali.
SHARE
No comments:
Post a Comment