TRA

TRA

Friday, June 23, 2017

Jafo akitaka kikundi cha DOYODO kuongeza ubunifu

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



DOY1
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwataka vijana kuwa mfano wa kuigwa Dodoma na nchi nzima katika kampeni yao ya kujiajiri wenyewe.
DOY2
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwasha mtambo wa kufyatulia matofali.
DOY3
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akishiriki kufyatua matofali katika mtambo huo.
DOY4
Naibu Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akizungumza na Wanafunzi waliokuwa wanafundishwa masomo ya ziada(tution) katika ofisi ya DOYODO.
DOY5
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na vijana wa taasisi ya DOYODO na Afisa Vijana kutoka Manispaa ya Dodoma alipokuwa anakagua miradi mbalimbali mapema leo ofisini kwao mjini Dodoma.
………………………………………………………………………………..
Naibu Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (TAMISEMI)Mhe.Selemani Jafo amewataka vijana wa Taasisi ya Maendeleo ya Vijana Dodoma(DOYODO) kuongeza ubunifu ili waweze kuwa washindani katika soko la biashara kwa kutumia fursa ya  wahamiaji wanaokuja Dodoma.
Mhe.Jafo aliyazungumza hayo alipokuwa anakagua miradi mbalimbali ya taasisi hiyo mapema leo na kuwataka kuwekeza kwenye kilimo  kwa kuwa   wanafikilia kupata eneo lao wenyenye ni vyema  kupata hekari moja kwa ajili ya kilimo cha mboga mboga na matunda kwani kinalipa.
’’Kumekuwa na tabia ya vijana kuchagua kazi na baadhi yao kusubiri kupata ajira kutoka Serikalini lakini nyie mmetoa mfano badala ya kutegemea ajira, mmejiajiri na ntahakikisha baadhi ya wabunge wanakuwa wa kwanza kuja kununua matofali hasa kwa wale wanaojenga Dodoma ’’
“Nitaongea na Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma ili mpatiwe milioni moja kutoka mfuko wa 5%ya makusanyo ya Manispaa ya Mapato ya vijana na milioni kumi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na mimi nachangia  kwa kununua matofali mia tano “Mhe.Jafo aliahidi.
Naye Afisa Mipango na Muhasibu wa DOYODO Elias Mbogo amesema taasisi inajipatia kipato chake kupitia vyanzo mbalimbali ikiwemo ada ya uanachama,tozo,miradi yao na misaada kutoka kwa wadau wa Taasisi.
Taasisi ya DOYODO imesajiliwa kisheria mwaka 2002 na kuanza kufanya shughuli zake rasmi toka 2015 na miradi waliyonayo ni mradi wa matofali,tuition(elimu),ufundi chelehani na kukodisha ukumbi kwa ajili ya semina na sherehe mbalimbali.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger