MEERUT, INDIA
Huwezi kuamini lakini ndivyo ilivyo. Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 8 na urefu wa futi 6 ameingia kwenye kitabu cha kumbukumbu (Guinness Book Record) kwa kile kinachoelezwa ndiye mrefu zaidi duniani.
Karan Singh kutoka Meerut nchini India ana historia nyingine kwa maana kuwa alizawa akiwa na uzito mkubwa pamoja na urefu pia. Urefu wake umekuwa gumzo kutoka kwa wanafunzi wenzake.
Urefu huo pia ulimshangaza mzazi wake, Dad Sanjay (41) huku akijipa moyo utamweka kwenye rekodi ya kipekee.
“Wakati Karan anazaliwa alikuwa na uzito wa kilo 7.8 na urefu wa sentimeta 63 kwa urefu. Hii ilimfanya aingie kwenye kumbukumbu wa kitabu cha rekodi.
"Hivyo alipofikisha miaka 5 aliweka rekodi ya kuwa na urefu mkubwa na sasa ana miaka 8. Kimsingi ameingia ameingia kwenye Guinness Records," alisema Sanjay.
SHARE
No comments:
Post a Comment