TRA

TRA

Thursday, June 22, 2017

Salah avunja rekodi ya dau la usajili Liverpool

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Liverpool wamekamilisha dili la usajili winga Mohamed Salah, kutoka As Roma ya Italia, kwa dau la Pauni million 39.

Usajili wa winga huyu umevunja rekodi ya usajili kwa wachezaji waliowahi sajiliwa na timu hiyo ambapo usajili wa gharama zaidi ulikuwa wa mshambuliaji Andy Carrol, aliposajiliwa kwa dau la pauni milioni 35 mwaka 2011.

Salah raia wa Misri mwenye umri wa miaka 25 amesaini mkataba wa miaka mitano kuweza kutumikia Liverpool.

 Salah amepewa jezi namba 11 aliyokua akivaa Roberto Firmino ambae kwa sasa atavaa jezi namba 9 

''Ninafuraha sana kuwepo hapa nitajitoa kwa asilimia mia moja na nitatoa kila kitu kwa ajili ya klabu hii, kiukweli nataka kushinda kitu nikiwa na timu hii", alisema Salah baada ya kukamilisha usajili huo.

CHANZO:BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger