Mamlaka
ya elimu ya ufundi Tanzania (VETA) kwa kushirikiana Kampuni ya simu za
mkononi ya Airtel kupitia application ya VSOMO leo wametangaza
na kuzindua kozi mpya za ufundi stadi za VETA zitakazotolewa kupitia
simu za mkononi ili kuwawezesha watanzania kujiunga na kupata utaalamu
na vyeti vya VETA kwa gharama nafuu.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dk. Bwire Ndazi akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kozi tano mpya kwenye awamu ya pili ya mpango wa kutoa mafunzo ya ufundi stadi kupitia programu ya VSOMO inayoratibiwa na kampuni ya Airtel, Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel, Beatrice Singano.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dk. Bwire Ndazi akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kozi tano mpya kwenye awamu ya pili ya mpango wa kutoa mafunzo ya ufundi stadi kupitia programu ya VSOMO inayoratibiwa na kampuni ya Airtel, Dar es Salaam jana. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel, Beatrice Singano.
Kozi
hizo mpya zinazoongezwa katika mfumo wa vsomo ni Huduma ya chakula na
mbinu za kuhudumia wateja, Matengenezo ya kompyuta,umeme
wa viwandani, ufundi Bomba wa Majumbani na Umeme wa magari.
Tangu
kuzinduliawa kwa mfumo huu wa mafunzo kwa njia ya mtandao kupitia
application ya VSOMO mwezi wa Juni 2016 ulianza
kutoa kozi mbalimbali za ufundi za VETA ikiwemo Ufundi umeme wa
manyumbani, Ufundi pikipiki, Ufundi wa simu za mkononi, Ufundi
Alluminium, Utaalamu wa maswala ya urembo pamoja ma Ufundi wa kuchomea
vyuma.
Lengo la mfumo huu likiwa ni kutimiza dhamira ya VETA
ya kutanua wigo wa mafunzo ya ufundi stadi nchini na kuongeza idadi ya
vijana kujipatia fani mbalimbali za ufundi ili waweze kuajirika au
kujiajiri. Mafunzo haya yanawawezesha wanafunzi kujisomea wakati wowote
kwa gharama nafuu kupitia simu zao za mkononi
za Airtel
Mfumo
huu wa masomo kwa njia ya Mtandao VSOMO, sasani maarufu kwa vijana
ambapo takwimu zinaonyesha zaidi ya vijana
30,000 tayari wamepakua application ya VSOMO, 8000 wamejiandikisha na
kati yao 50 wanasoma kozi mbalimbali zilizopo pia wapo waliomaliza na
kupata vyeti vya VETA.
Akiongea
wakati wa kuzindua na kutangaza kozi hizo, Mkuu wa Chuo cha Veta
Kipawa, Mhandisi Lucius Luteganya alisema “mafunzo ya ufundi
kwa njia ya mtandao ya VSOMO yametuwezesha kuongeza wigo na kuwafikia
watanzania wengi nchini. Tunaamini bado tunayofursa ya kuongeza wigo
zaidi na kuongeza idadi ya vijana wenye ueledi ili kwenda sambamba na
agenda ya serikali ya awamu tao ya uchumi wa viwanda
kwa kupata nguvu kazi yenye taaluma muhimu katika kuendesha uchumu wa
nchi”
“Tunaamini kozi hizi mpya zitatawavutia vijana wengi kujiandikisha, kusoma na kupata ujuzi zaidi.” Alisisitiza Eng Luteganya
Luteganya alisema kuwa “Ili kupata mafunzo ya VSOMO kupitia Airtel,
ukiwa na Airtel pakua application katika google play store,
na kujisajiri na kisha chagua kozi inayokidhi mahitaji yao. ili
kuhakikisha tunasimamia viwango vya elimu vilivyowekwa na VETA, wale
watakaomaliza masomo yao nadharia kupitia VSOMO watafanya mtihani ili
kufaulu na kujiunga na mafunzo ya vitendo katika vituo
vya VETA vilivyopo nchi nzima. Vyeti vya kuhitimu mafunzo vitatolewa
kwa wale watakaofaulu mafunzo katika hatua zote mbili ya nadharia na
vitendo”.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano
Mallya alisema “Tunajisikia furaha kuongeza kozi nyingi zaidi
katika mfumo huu wa masomo kwa njia ya mtandao wa VSOMO kwani
itatuwezesha kufikia idadi kubwa ya vijana wanaosoma kwa kupitia simu
zao za mkononi. Lengo letu ni kuhakikisha tunakuwa na kozi nyingi ili
kwenda sambamba na matarajio na mahitaji ya wanafunzi
na watanzania kwa ujumla"
SHARE
No comments:
Post a Comment