TRA

TRA

Saturday, June 10, 2017

ZANTEL YATOA MSAADA WA SARUJI NA MABATI KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO WA MKOA WA KUSINI PEMBA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !





Mkuu wa Kampuni ya mawasiliano ya Zantel-Zanzibar, Bw. Mohamed Khatib Baucha (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mwanajuma Majid Abdallah mifuko ya Saruji kwa kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni katika mkoa huo. Zoezi la makabidhiano ya msaada huo lilifanyika jana mkoani humo ambapo Zantel walitoa jumla ya mabati 350 na Saruji mifuko 350, vyote vikigharimu Sh. 13 milioni.




Mkuu wa Kampuni ya mawasiliano ya Zantel-Zanzibar, Bw. Mohamed Khamis Baucha (kushoto) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mwanajuma Majid Abdallah mabati kwa kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni katika mkoa huo. Zoezi la makabidhiano ya msaada huo lilifanyika jana kisiwani Pemba-Zanzibar ambapo Zantel walitoa jumla ya mabati 350 na Saruji mifuko 350, vyote vikigharimu Sh. 13 milioni.



Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mwanajuma Majid Abdallah akiwakabidhi wakuu wa wilaya za mkoa huo mabati yalitolewa na Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel kwa ajili ya waathirika wa mafuriko yaliyotokea hivi karibuni katika mkoa huo. Zoezi hilo lilifanyika jana kisiwani Pemba-Zanzibar ambapo jumla ya mabati 350 na Saruji mifuko 350 kwa pamoja vilikabidhiwa na Kampuni ya Zantel. (Katikati) ni Mkuu wa Wilaya ya Chakechake Mhe. Salama Mbarouk Khatib na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Mkoani Mhe. Hemed Suleiman Abdallah.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kusini Pemba, Ndg. Yussuf Mohammed Ali (kushoto) akimtambulisha Mkuu wa Zantel-Zanzibar, Bw. Mohamed Khamis Baucha (wa pili kushoto) kwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mhe. Mwanajuma Majid Abdallah (hayupo pichani) kabla ya Mkuu huyo wa Zantel kukabidhi msaada wa Saruji na Mabati kwa ajili ya waathirika wa mafuriko mkoani humo. Msaada huo una gharama ya Sh 13 milioni na lilifanyika jana kisiwani Pemba-Zanzibar. Wa tatu Kulia ni Ofisa wa fedha na Utawala wa Tawi la Zantel–Pemba, Yakoub Fadhil Juma.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger