TRA

TRA

Monday, July 10, 2017

Ziara ya Waziri Ummy Mwalimu kituo cha afya Katoro mkoani Geita

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 
KATO1
Waziri Ummy akimsalimia mtoto aliyefika kituoni na  mama yake kupata huduma ya afya, Waziri huyo amefika katika  kituo hicho ili kujionea hali ya kituo hicho ambacho kinahudumia idadi kubwa ya wakazi wa mji huo pamoja na jirani zake licha ya kuwa na changamoto ya watumishi pamoja na miundombinu ili  kuwezesha  vituo vya afya nchini kote vinafikia malengo ya serikali katika kuboresha afya na huduma za afya kwa watanzania.
KATO2
Moja ya Vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano ni Upatikanaji wa Dawa kwenye vituo vyote vya Serikali,Waziri Ummy Mwalimu akiongea na watoa huduma kwenye dirisha la dawa katika kituo hicho.
KATO3
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akimfafanulia jambo mmoja wa wagonjwa waliofika kupata huduma kwenye kituo cha afya cha Katoro
KATO4
Waziri Ummy akitoa maelekezo kwenye matangazo yaliyobandikwa kwenye kuta za kituo hicho,kushoto ni Mkurugenzi wa HALMASHAURI YA Geita Lawrence Kalabezile.Waziri huyo amewataka watumishi wa kituo hicho kujituma na kutimiza wajibu wao katika kuwahudumia wananchi hususan katika kuokoa maisha ya wagonjwa.
KATO5
Katika ziara hivyo Waziri Ummy alikagua ujenzi wa jengo la upasuaji wa dharura unaojengwa kwenye kituo hicho.Waziri wa Afya yupo  katika ziara ya kikazi ya  siku tatu Mkoani Geita (PICHA ZOTE NA WIZARA YA AFYA)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger