TRA

TRA

Saturday, August 12, 2017

China yamuonya Trump kuchunga matamshi

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Rais wa China Xijinping amemtaka rais Donald Trump kuchunga mtamshi na vitendo vinavyozidisha hali ya kuzua wasiwasi ,chombo cha habari cha kiserikali kimeripoti.

 Rais Xi Jinping

Rais Trump na Korea Kaskazini wamekuwa wakirushiana cheche za maneno huku rais rais huyo wa Marekani akionya kuikabili kivita vikali Korea Kaskazini.

Lakini China ambaye ni mshirika mkuu wa Korea Kaskazini ametaka pande zote mbili kuwa na uvumilivu.

Taarifa ya ikulu ya Whitehouse imesema kuwa Marekani na China zilikubaliana kwamba Korea Kaskazini inafaa kusitisha uchokozi na tabia mbaya.

Hofu kubwa inayoendelea kutanda kuhusu mpango wa kinyuklia wa Korea Kaskazini ilizidi baada ya taifa hilo kufanyia majaribio makombora yake ya masafa marefu mnamo mwezi Julai.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger