TRA

TRA

Saturday, August 12, 2017

YANAYOJIRI UCHAGUZI MKUU WA TFF KUTOKA DODOMA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

SHUGHULI za Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) zimeanza rasmi katika Ukumbi wa St. Gaspel mjini Dodoma ambapo wajumbe kutoka kanda 13 za shirikisho hilo hapa nchini, pamoja na wagombea wa nafasi mbalimbali wamehudhuria.


Waziri Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa na viongozi wa uchaguzi wa TFF kwenye mkutano huo.
Uchaguzi huo umetanguliwa na Mkutano Mkuu wa TFF ambao umezinduliwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe ukiwa na ajenda 14 zikiwemo kutambulisha wajumbe, kupitisha wagombea na ajenda ya uchaguzi.
Wajumbe wa mkutano huo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mkutano huo, Dkt. Mwakyembe amewasisitiza wajumbe wanaoshiriki uchaguzi huo kuzingatia kanuni za utawala bora ili kuleta tija katika maendeleo ya soka hapa nchini.
Hali ilivyokuwa ukumbini.

Waliohudhuria uchaguzi huo ni pamoja na Makamu Rais wa TFF, Wallace Karia, Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, Salum Madadi, pia wajumbe wa CAF na Fifa ambao wameona mchakato wa uchaguzi utachelewa kulingana na jinsi mipangilio yao ilivyo, hivyo na wao wameshauri mkutano ufanyike haraka ili waanze shughuli ya uchaguzi mara moja.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger