
Miss Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu.
MIAKA ya hivi karibuni mrembo ambaye ni kipenzi cha watu na Mshindi wa Shindano la Miss Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu amekuwa kimya, hasikiki sana kwenye media tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma.
Staa wa Filamu Bongo, Batuli.
Si
mtu wa kuonekana viwanja tena hovyo, kujiachia na marafiki na hata
ukitazama kwenye mitandao yake ya kijamii anachagua kwa sasa picha ipi
ya kuposti ambapo picha anazoweka nyingi kwa sasa ni zile anazokuwa
lokesheni ama kwenye shughuli maalum za kijamii na kwa uchache picha za
baadhi ya washikaji zake.
Picha
ambazo zinaonesha kukiuka maadili hatupii tena kama awali. Unaweza
kusema pengine ni kwa sababu ameingia kwenye siasa ambapo miezi ya hivi
karibuni alitangaza kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Staa wa Filamu Bongo, Kajala Masanja.
Hata
hivyo kitambo tu alikuwa anashiriki kwenye siasa lakini hakuwa mkimya
kama ilivyo hivi sasa. Ukiachana na hayo, vipi kuhusu marafiki zake
‘wabeba mikoba?’ Wale aliokuwa anakula nao bata mpaka kuku wanaona wivu,
wako wapi? Wamejichimbia chimbo gani kwa sasa?
Aunt Ezekiel.
Mbona
hawaambatani naye na kuonekana naye kama ilivyokuwa awali? Ama nao
wamepotea kwa sababu Wema amekuwa si mtu wa kiki kiivyo kwa sasa
kutokana na kuishi maisha yenye ‘limit’? Ninapozungumzia wabeba mikoba
wa Wema wengine wanaweza kuwa hawajawaelewa sawasawa. Wanaweza kujiuliza
ni kina nani? Ngoja nikwambie; Baadhi yao ni kina Aunt Ezekiel, Jike Shupa, Muna, Kajala Masanja, Snura, Jack wa Chuz na Batuli. Hao walikuwa ni washikaji zake kwelikweli.
Kila
kona Wema alipokuwa walikuwepo. Wengine walikula na kulala naye
chumbani pamoja. Mfano Aunt Ezekiel. Kila mara alikuwa nyumbani kwa Wema
na liliwahi kuibuka varangati kati ya Aunt na aliyekuwa meneja wa Wema,
Martin Kadinda, baada ya muigizaji huyo kulala nyumbani kwa Wema na
Kadinda kumkuta. Kitendo hicho Kadinda alionekana kutokukifurahia
akalianzisha vurumai na pia alikuwa akimshutumu Aunt kuwa ndiye chanzo
cha ugomvi wa Wema na Kajala.
SHARE











No comments:
Post a Comment