Malkia
wa filamu bongo, Jacqueline Wolper amefunguka na kusema hawezi kutoka
kimapenzi na wanaume ambao wameoa kwa madai anahofia wanaweza
wakatelekeza familia zao kwa maana yeye akichukua kitu huwa hawi
lelemama hata kidogo.
Wolper amebainisha hayo wakati kusema amekuwa muoga sana kufanya jambo hilo kwa kuwa anaogopa laana.
"Nakuwa
naogopa sana, nawaheshimu sana kwa sababu wengi wao wanakuwa ni waume
za watu halafu hakuna laana mbaya kama kutembea na mume wa mtu,
'otherwise' ukute huyo mtu anasumbuliwa na mke wake unajua kuna wanawake
ni wakorofi tu wanakuwa wanawasumbua waume zao na kupelekea kutafuta
pumziko nje labda itokee hivyo lakini hivi hivi naona kama ni baba
yangu", alisema Wolper.
Pamoja na hayo, Wolper ameendela kwa kufafanua baadhi ya mambo kwa kusema "No
siongelei umri hapa naongelea imani, kwa sababu mimi nikimchukua mume
wa mtu sitokuwa lele mama halafu sasa kule nyumbani kwake atakuwa
anapunguza mapenzi kwa hiyo kidogo nakuwa na huruma na ndiyo maana mimi
nataka niwe na cha kwangu sitaki kuiba cha mtu".
Katika
siku za hivi karibuni Jacqueline Wolper amekuwa akiandamwa sana katika
skendo la kutoka na wanaume wadogo kiumri japo yeye mwenyewe amekuwa
mgumu kuweka bayana kuhusiana na mambo hayo ambayo wanazungumziwa
mtaani.
SHARE
No comments:
Post a Comment