TRA

TRA

Monday, September 25, 2017

TP MAZEMBE YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !




tp_mazembe_onze_2017-750x410
Mabingwa watetezi wa Kombe la Shirikisho barani Afrika timu ya TP Mazembe  imetinga hatua ya nusu Fainali kwa kushindo ya Michuano ya Shirikisho baada ya kuwatandika Waarabu wa Sudan,Al-Hilal Obeid kwa mabao 5-0 na kuwatupa nje kwa jumla ya magoli 7-1.
TP Mazembe wakiwa kwenye dimba lao la Stade Fredric Kibassa Maliba lilipo Mjini Lubumbashi waliingia uwanjani wakiwa na ushindi magoli 2-1 ambao waliupata Sudan wiki iliyopita.
Alikuwa beki kisiki wa Mazembe Jean Kassusla aliwanyanyua mashabiki waliokuwa wamejaa kwa kuishangilia timu yao dakika ya 39 akifunga bao kwa mkwaju Mkali wa Mita 18 na kumshinda Mlinda mlango wa Al-Hilal hadi mapumziko Wenyeji walikuwa mbele kwa bao 1-0.
_97994836_457319028
Jean Kassusla akipiga Mpira wa adhabu ulioenda moja kwa moja hadi golini.
Kipindi cha pili kilikuwa kigumu kwa Wasudan hao kwani waliweza kutandikwa bao nne huku wakizidiwa kila idara na Mazembe wakicheza kwa kushambulia lango kama nyuki dakika ya 49 Mshambuliaji raia Wa Mali,Adama Traore alifunga bao la pili na dakika tano Ben Malango alipigilia Msumari wa tatu.
Akitokea benchi Mshambuliaji wa Congo,Elia Meshak aliifungia Mazembe bao la nne kwa kuwachambua mabeki wa Al-Hilal kabla ya kuachia shuti kali huku wakiwa wanajiuliza beki kisiki Issam Mpeko aliupigilia chuma cha tano na kuweza kuwanyamazisha Waarabu hao na kutupwa nje ya hatua ya nane bora.
Kwa Matokeo hayo TP Mazembe wametinga hatua ya Nusu Fainali  la Shirikisho barani Afrika huku wakisaka nafasi ya kuchukuwa kombe hilo kwa mara ya pili Mfululizo ikumbukwe hao ndo mabingwa watetezi na watakutana na timu ya FUS Rabat ya Morocco ambao nao walitinga Nusu baada ya kuwachapa Watunisia timu ya CS Sfaxien kwa jumla ya mikwaju 4-3 ya Penalti.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger