TRA

TRA

Sunday, November 5, 2017

BODI YA MIKOPO YATOA ORODHA NYINGINE YA WANAFUNZI WALIOPATA MIKOPO

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HELSB) imetoa orodha ya awamu ya tatu ya wanafunzi 7,901 wa mwaka wa kwanza watakaopata mikopo.
Taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya bodi na kuthibitishwa na Meneja Mawasiliano wa HELSB, Omega Ngole imesema hadi sasa wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo ni 29,578. Bodi ilisema jumla ya wanafunzi 30,000 watapata mikopo hiyo.
Katika awamu ya kwanza wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza walipata mikopo na awamu ya pili wanafunzi 11,481 walipata.
Ngole akizungumza na Mwananchi leo Jumapili Novemba 5,2017 amesema orodha ya wanafunzi waliopata mikopo inapatikana www.heslb.go.tz.
Amesema bado bodi inaendelea kuchambua majina ya wanafunzi wengine walioomba na taarifa zitatolewa baadaye.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger