TRA

TRA

Monday, November 6, 2017

Dionatan Teixeira: Beki wa zamani wa Stoke afariki akiwa na miaka 25

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Teixeira aliumia mguuni msimu wake wa kwanza Stoke kabla ya mkataba wake kutamatishwa Januari 

Beki wa zamani wa Stoke City Dionatan Teixeira amefariki dunia akiwa na miaka 25 kutokana na kile akinachoaminika kuwa mshtuko wa moyo.

Alijiunga na Stoke 2014 baada ya kufanyiwa majaribio klabu kadha za Ligi ya Premia ikiwemo Manchester City.
Lakini mchezaji huyo wa Brazil hakufanikiwa England kwani alitatizwa na majeraha.

Alichezea Stoke mechi mbili pekee, kama nguvu mpya katika miaka mitatu aliyokaa Stoke.

Teixeira alikuwa Brazil alipougua na kufariki Jumapili, kwa mujibu wa klabu yake aliyokuwa anaichezea FC Sheriff, ya Moldovia ambayo inacheza ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League msimu huu.

Klabu hiyo ilishinda ligi nchini humo pamoja na kombe la ligi.
FC Sheriff wamesema: "Atasalia daima katika nyoyo zetu."

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger