
Mkurugenzi wa Kampuni ya
Udalali ya Msama Auction Mart Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi wa
habari jana katika kituo cha Polisi Kanda Maalum Dar es salaam kabla ya
kuanza kwa msako huo.
………………………………………………………………
Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi,
Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo imeendelea na zoezi la ukamataji wa Wadurufu wa kazi za sanaa na
wakwepa kodi kupitia kazi hizo.
Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo imeendelea na zoezi la ukamataji wa Wadurufu wa kazi za sanaa na
wakwepa kodi kupitia kazi hizo.
Zoezi hilo limeendelea katika sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam ambapo pia imesisitizwa kuendelea nchi nzima.
Akizungumza na Waandishi wa
Habari kabla ya kuanza kwa shughuli hiyo, Mkurugenzi wa Msama Auction
Mart amewaasa Wafanyabiashara wote kufuata taratibu
kuhakikisha wanauza bidhaa zenye Stika ya TRA.
“Uzeni bidhaa zenye Stika ya TRA, acheni kuwaibia Wasanii, wakati huu ni wakati wa
Serikali kupata haki yake na Wasanii pia wapate haki zao,wafaidi jasho
la kazi yao”, amesema Msama
Pia amewaasa Watanzania
wanaonunua kazi hizo za sanaa kuacha kununua kazi ambazo hazina Stika
ya TRA, amesema Watanzania wanapaswa kujifunza kulipa Kodi kupitia kazi
hizo zenye Stika halali ya TRA.
“Wale wanaoburn CD,
Wanaoingiza nyimbo kutumia Kompyuta muache, zoezi hili sio Dar es Salaam
pekee zoezi ni la nchi nzima na tutahakikisha kila anayenunua bidhaa
hizo ananunua bidhaa zenye Stika”, amesisitiza Msama.


Baadhi ya Wafanyakazi wa
kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart na askari wakiwa wamevamia
moja ya duka linalofanya biashara ya kuuza kazi za Wasanii kwa
maeneo ya Kariakoo jana jijini Dar.
maeneo ya Kariakoo jana jijini Dar.

Baadhi ya wauziaji wa CD hizo
wamefuata utaratibu wa kuuza CD zenye Stika za TRA kama huyu muuzaji
ambaye alikutwa akiuza CD zake zenye Stika eneo la Buguruni jana.

Baadhi ya wafanyakazi wa
Kampuni ya Msama Auction Mart pamoja na polisi wakipita katika maduka
mbalimbali eneo la Buguruni kukagua na kukamata CD ambazo hazina stika
za TRA.
SHARE
No comments:
Post a Comment