TRA

TRA

Sunday, November 5, 2017

LAPF HAINA MCHEZO KIUTENDAJI. YAKABIDHI MAKONDA MILIONI 5 UJENZIOFIFI ZA WALIMU

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 
001
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akipokea Msaada wa Fedha Taslimu Sh. Milioni 5 kutoka kwa James Mlowe Meneja Mawasiliano na Masoko Mfuko wa Pensheni wa LAPF kwa ajili ya kununulia mifuko 500 ya saruji katika kuchangia kampeni ya ujenzi wa Ofisi za Kisasa za walimu katika shule za Msingi na Sekondari Mko wa Dar es salaam.
Kampeni hiyo imeanzishwa na Mkuu wa mkoa wa Mh.Paul Makonda katika jijini la Dar es salaam, ambapo  Ofisi zaidi ya 400 zitajengwa katika shule za jiji la Dar es salaam hivyo  kuboresha utendaji kazi wa waalimu hao, Kalia anayeshuhudia tukio hilo  ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi Kanali Charles Mbuge, Makabidhiano hayo yamefanyika mwishoni mwa wiki ofisini kwa Mkuu wa mkoa.
01
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akimsikiliza Bw. James Mlowe Meneja Mawasiliano na Masoko Mfuko wa Pensheni wa LAPF wakati akizungumza kabla ya kukabidhi msaada uliotolewa na LAPF   kwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za walimu katika shule za sekondari na Msingi katika mkoa wa Dar es salaam.
2
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akizungumza  katika makabidhiano hayo yaliyofanyika Ofisini kwake katikati ni  Bw. James Mlowe Meneja Mawasiliano na Masoko Mfuko wa Pensheni wa LAPF na kulia ni Kanali Charles Mbuge Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi.
3
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akisisitiza jambo wakati akizungumza  katika makabidhiano hayo yaliyofanyika Ofisini kwake lulia ni  Bw. James Mlowe Meneja Mawasiliano na Masoko Mfuko wa Pensheni wa LAPF.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger