TRA

TRA

Tuesday, November 7, 2017

MAVUNDE AWAPA NEEMA WAJASIRIAMALI DODOMA MJINI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana Anthony Mavunde ambaye pia ni Mbunge wa Dodoma mjini leo amefungua semina ya wajasiriamali wapatao 2000 wa Jimbo hilo.

Semina hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Cavilam wilayani Dodoma ambapo wajasiriamali hao watapata nafasi ya kujifunza juu ya elimu ya Ujasiramali na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali.

Aidha amesema kupitia semina hiyo watatoa walimu 205 ambao watazunguka katika kata zote 41 za Dodoma Mjini kwenda kufundisha vikundi vya wakinamama,Vijana na Wazee katika masuala ya utengenezaji bidhaa na kuongeza thamani,Ufugaji wa Kuku, Samaki na Mafunzo ya kilimo Bora.

Mavunde amesema baada ya kukamilika kwa mafunzo hayo litaandaliwa kongamano lingine kubwa litakalohusisha Taasisi za fedha na Mifuko ya Uwezeshwaji ili wajasiriamali wapate fursa ya kufahamu namna ya kuifikia mikopo na ruzuku zitakazosaidia upatikanaji wa mitaji ya kufanyia shughuli za uzalishaji mali.
 Mbunge wa Dodoma mjini na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Anthony Mavunde akifungua semina ya wajasiriamali Dodoma.
 Mbunge wa Dodoma mjini na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Anthony Mavunde akizungumza na wajasiriamali.
Washiriki wa semina ya ujasiriamali

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger