TRA

TRA

Saturday, November 11, 2017

Upasuaji wa Samatta wamalizika aalama

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


20171110_201501-640x475
Ni taarifa njema kwa watanzania wote hususan wadau wa soka kwamba, nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta upasuaji wake wa goti umefanyika na kumalizika salama.
Samatta aliumia goti November 4, 2017 wakati akiitumikia klabu ya ya KRC Genk ya Ubelgiji na kushindwa kuendelea na mechi dhidi ya Lokeren mchezo ambao ulimalizika kwa suluhu.
Kupitia ukurasa wake rasmi wa wa instagram (samagoal77) ameandika ujumbe unaothibisha kwamba upasuaji umefanyika na kumalizika salama.
“Napenda kuwajulisha kuwa, upasuaji wangu umeenda vizuri. Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, timu ya madaktari pamoja na mashabiki wangu.”
“Nimepokea meseji nyingi sana kutoka sehemu tofauti duniani na napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru sana kwa meseji na Dua zenu.”
Baada ya kufanyiwa vipimo, madaktari walimwambia Samatta atakaa nje ya uwanja kwa takribani wiki sita kabla ya kuanza kucheza tena.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger