TRA

TRA

Tuesday, November 7, 2017

ZOEZI LA USAJILI VITAMBULISHO VYA TAIFA LASHIKA KASI MKOANI SINGIDA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Singida_01
Mkuu wa Kitengo cha Biashara Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa – NIDA Ndugu Thomas William pamoja na Ndugu Innecent Baraza Meneja Usimamizi wa Majengo (Kushoto) wakifuatilia kwa karibu Uingizwaji wa taarifa za waombaji wa Vitambulisho vya Taifa wakati wa Zoezi la Usajili na Utambuzi linaloendelea Mkoa wa Singida.
Singida_02
Wanachi katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida, wakifanyiwa usajili wa Maombi ya Vitambulisho vya Taifa katika zoezi la Usajili wa Mkupuo (Mass Registration) linaloendela hivi sasa Mkoani humo.
Singida_03
Baadhi ya Wananchi katika kata ya Kindai Halmashauri ya Manispaa Singida wakiwa kwenye foleni kuelekea kwenye chumba cha uchukuaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya kielektroniki.
Singida_04
Baadhi ya Wananchi katika kata ya Kindai Halmashauri ya Manispaa Singida wakiwa kwenye foleni kuelekea kwenye chumba cha uchukuaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya kielektroniki.
Singida_05
Baadhi ya Wananchi katika kata ya Kindai Halmashauri ya Manispaa Singida wakiwa kwenye foleni kuelekea kwenye chumba cha uchukuaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya kielektroniki.
Singida_06
Baadhi ya Wananchi katika kata ya Kindai Halmashauri ya Manispaa Singida wakiwa kwenye foleni kuelekea kwenye chumba cha uchukuaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya kielektroniki.
…………………………………………………………………..
Usajili Vitambulisho vya Taifa mkoani Singida umezidi kushika kasi wananchi wakifika kwa wingi kupata huduma ya Usajili unaohusisha uchukuaji wa alama za Kibiolojia, picha na  Saini ya Kielektroniki.
Kwa kushirikiana kwa karibu na Maafisa Usajili, Watendaji wa Kata na Serikali za Mtaa, watumishi wa Mamlaka wamekuwa wafakifanya jitihada kubwa za kuhakikisha Wananchi wanatambua umuhimu wa kuwa na Vitambulisho vya Taifa pamoja na Matumizi yake Msingi na kushiriki kikamilifu kujisajili.
Pamoja na misururu mirefu wananchi hao wameonyesha kutokata tamaa kwa foleni ndefu badala yake wamekuwa wakihamasishana kushiriki ili kila mmoja kupata haki yake msingi kusajiliwa.
Mkoa wa Singida ni miongoni mwa mikoa 12 ya Tanzania ambayo zoezi hilo linaendelea kwa sasa ukiwemo mkoa wa Mbeya, Njombe, Songwe, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Geita na Iringa.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger