Waziri wa Maji na Umwagiliaji,
Mhandisi Isack Kamwelwe akimkaribisha ofisini mgeni wake, Balozi wa
Uholanzi nchini, Jeroen Verheul mara baada ya kuwasili.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akiwa kwenye mazungumzo na Balozi wa Uholanzi nchini, Jeroen Verheul.
………………..
Waziri wa Maji na Umwagiliaji,
Mhandisi Isack Kamwelwe amekutana na Balozi wa Uholanzi nchini, Jeroen
Verheul na kufanya nae mazungumzo kuhusu mpango wa kukamilisha mradi wa
maji wa kitaifa wa Handeni (HTM) uliopo katika wilaya za Handeni na
Korogwe, mkoani Tanga.
Mazungumzo hayo yaliyofanyika
kwenye ofisi za wizara za Ubungo Maji, Jijini Dar es Salaam, yalilenga
katika kutatua changamoto za mradi huo ili uweze kukamilika na kutoa
huduma kwa ufanisi kwa wakazi ambao kwa sasa wamefikia 300,000
kulinganisha na 180,000 kama lengo la awali katika vijiji 79 vya wilaya
za Handeni na Korogwe.
Katika kikao hicho Waziri Kamwelwe
na Balozi Verheul walikubaliana hatua za haraka zichukuliwe kwa lengo
la kuondoa vikwazo vyote na kutekeleza mpango huo mara moja.
SHARE
No comments:
Post a Comment