TRA

TRA

Monday, March 28, 2016

TAMASHA LA PASAKA LAPAGAWISHA MASHABIKI WA MUZIKI WA INJILI MWANZA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


1
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akizindua rasmi albam mpya ya mwimbaji Goodluck wakati wa tamasha la Pasaka lililofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Mwanza , Wabunge pamoja na Maaskofu wa makanisa ya Mwanza.
Tamasha hilo ambalo limehudhuriwa na mashabiki wengi mkoani humo limetumbuizwa na waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili kutoka hapa nchini na nchi jirani za Zambia na Kenya, waimbaji hao ni Upendo Nkone , Martha baraka , Jesca BM, Joshua Mlelwa , Tumsifu Rufutu, Christopher Mwahangila, Jeniffer Mgendi, Bonny Mwaiteje, Goodluck ambaye amezindua albam yake mpya na waimbaji Faustine Munishi kutoka nchini Kenya, Solomon Mukubwa kutoka Nchini Kenya pamoja na Ephraim Sekereti kutoka nchini Zambia wote kwa pamoja wamefanya maonesha mazuri yaliyopagawisha mashabiki wa muziki wa injili katika uwanja wa CCM Kirumba na kuwafanya wacheze kila wakati, katika picha kulia ni mwimbaji Goodluck na kushoto ni Bw. Alex Msama Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion inayoandaa matamasha hayo.
Tamasha hilo litaendelea kesho kwa onesho kabambe linalotarajiwa kufanyika  mjini Kahama mkoani Shinyanga baada ya kumaliza maonyesho  mawili katika mikoa ya Geita na Mwanza.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-MWANZA)
2
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye wa nne kutoka kulia  akimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela alipokuwa akimkaribisha rasmi ili kutoa salam zake kutoka kwa serikali.
3
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akishiriki katika sala maalum ya kuombea albam ya mwimbaji Goodluck  wa pili kutoka kulia iliyotolewa na maaskofu wa mwanza kabla ya kuizindua
4
Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Nape Nnauye akishuka kutoka jukwaani kwa ajili ya kuizindua rasmi albam hiyo na kutoa salaam za serikali katika tamasha la Pasaka.
5
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela akipokewa na Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mh. Baraka Konisaga kushoto na Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama wakati alipowasili kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
6
Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mh. Baraka Konisaga akipokewa  na Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama wakati alipowasili kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.(P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger