TRA

TRA

Wednesday, April 20, 2016

SERIKALI KUENDELEA KULINDA KAZI ZA WASANII NCHINI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



FIS1
Mkurugenzi wa Elimu kwa mlipa kodi toka Mamlaka ya Mapato    Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo akionesha kwa waandishi wa Habari leo Jijini Dar es salaam moja ya CD zilizokamatwa wakati wa msako wa kubaini wale wote wanaojihusisha na uuzaji na usambazaji wa kazi za wasanii bila kuwa na stempu za kodi katika bidhaa za filamu na muziki. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi Joyce Fissoo na mwisho kulia ni Afisa Habari wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bi Mariam Mwayera.
FIS2
Mkurugenzi wa Elimu kwa mlipa kodi toka Mamlaka ya Mapato    Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo (katikati) akitoa wito leo Jijini Dar es salaam  kwa wasambazaji na wauzaji wa kazi za Filamu na muziki kuzingatia sheria na Kanuni zinazosimamia sekta hiyo kwa kuwa Serikali itawachukulia hatua kali wale wote watakaoenda kinyume cha sheria na taratibu zilizopo ikiwemo kutozwa faini isiyopungua milioni tano au kifungo kisichopungua miaka mitatu jela. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi Joyce Fissoo,Kushoto ni Afisa Utamaduni wa Bodi ya filamu Bw. Wilhadi Tairo.
FIS3
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi Joyce Fissoo akifafanua kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu mikakati ya Bodi hiyo kuhakiksha kuwa kazi za wasanii wa filamu zinaendana na maadili ya Taifa.kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Richard Kayombo.(P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger