
Mkurugenzi
wa Elimu kwa mlipa kodi toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw.
Richard Kayombo akionesha kwa waandishi wa Habari leo Jijini Dar es
salaam moja ya CD zilizokamatwa wakati wa msako wa kubaini wale wote
wanaojihusisha na uuzaji na usambazaji wa kazi za wasanii bila kuwa na
stempu za kodi katika bidhaa za filamu na muziki. Kulia ni Katibu
Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi Joyce Fissoo na mwisho kulia ni Afisa
Habari wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bi Mariam Mwayera.

Mkurugenzi
wa Elimu kwa mlipa kodi toka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw.
Richard Kayombo (katikati) akitoa wito leo Jijini Dar es salaam kwa
wasambazaji na wauzaji wa kazi za Filamu na muziki kuzingatia sheria na
Kanuni zinazosimamia sekta hiyo kwa kuwa Serikali itawachukulia hatua
kali wale wote watakaoenda kinyume cha sheria na taratibu zilizopo
ikiwemo kutozwa faini isiyopungua milioni tano au kifungo kisichopungua
miaka mitatu jela. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi Joyce
Fissoo,Kushoto ni Afisa Utamaduni wa Bodi ya filamu Bw. Wilhadi Tairo.

Katibu
Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi Joyce Fissoo akifafanua kwa waandishi wa
habari leo jijini Dar es salaam kuhusu mikakati ya Bodi hiyo kuhakiksha
kuwa kazi za wasanii wa filamu zinaendana na maadili ya Taifa.kushoto ni
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania Bw. Richard Kayombo.(P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment