







Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema
Serikali ipo katika hatua za mwisho kuanza mradi wa ujenzi wa barabara
ya Tabora-Koga-Mpanda yenye urefu wa Km. 356 kwa kiwango cha lami ikiwa
ni utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano aliyoitoa kwa wananchi
wa Mikoa ya Katavi na Tabora.
Ametoa
kauli hiyo wilayani Sikonge mkoani Tabora, mara baada ya kukagua
barabara hiyo ambapo pamoja na mambo mengine amesema ujenzi huo
unatarajia kuanza rasmi hivi karibuni.
‘Ujenzi
wa barabara hii tumeugawa katika sehemu tatu ili kuharakisha
utekelezaji wake, tutahakikisha ifikapo mwisho wa mwaka huu, makandarasi
wote watatu watakuwa katika maeneo yao ya kazi’, amesema Prof. Mbarawa.
Amesisitiza
kuwa wananchi wanaostahili kulipwa fidia watalipwa kwa wakati kwa kuwa
takribani shilingi bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.
Prof.
Mbarawa pia amekagua daraja la Koga linalounganisha Mkoa wa Katavi na
Tabora na kuwataka viongozi wa mikoa hiyo kuhakikisha kuwa magari
yasiyozidi tani tatu ndio yanayopita katika daraja hilo ili kuepusha
ajali hadi ukarabati mkubwa utakapofanyika.
Naye
Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Kanali Mstaafu Issa Nziku amemuomba Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kupandisha hadhi baadhi ya barabara
katika Wilaya hiyo ili zihudumiwe na Wakala wa Barabara nchini
(TANROADS), kutokana na uwezo mdogo wa Halmashauri hiyo kuzikarabati
kila wakati.
Katika
Hatua nyingine Prof. Mbarawa amekagua uwanja wa Ndege wa Tabora na
kuwataka viongozi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) na Mamlaka ya
Usafiri wa Anga Tanzania(TCAA) kuangalia namna bora ya ukarabati wa
kiwanja hicho ili uruhusu ndege kubwa kutua na kuongeza biashara.
Prof.
Mbarawa yuko katika ziara ya siku saba ya kukagua miundombinu ya
taasisi zilizo chini ya Wizara yake katika mikoa ya Magharibi ili
kuifungua kanda hiyo kimiundombinu na hivyo kufufua fursa za kiuchumi.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
SHARE
No comments:
Post a Comment