TRA

TRA

Thursday, July 28, 2016

MWENYEKITI WA BODI YA JKCI , PROFESA WILLIAM MAHALU APONGEZA UTENDAJI WA JKCI.

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


jki1Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete-JKCI- Profesa William Mahalu( katikati) akiwasili ndani  taasisi hiyo kwa mara ya kwanza tangu ateuliwe na Rais John Magufuli  , kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI , Profesa Mohamed Janabi  na  kulia ni Afisa Uhusiano wa Taasisi hiyo Maulid Kikondo.
jki2Profesa William Mahalu akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.
jki3Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Profesa Mohamed Janabi akielezea utendaji kazi wa taasisi hiyo .
jki4Mwenyekiti wa Bodi ya JKCI Profesa William  Mahalu akijitambulisha kwa viongozi wa taasisi hiyo .
jki5Baadhi ya viongozi wa Taasisi ya JKCI wakimsikiliza Profesa Mahalu wakati akizungumza nao mara baada ya kujitambulisha .
……………………………………………………………………………………………….
Dar es salaam,
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Moyo ya Jakay Kikwete JKCI- Profesa William Mahalu kwa mara ya kwanza tangu ateuliwe na Rais John Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya taasisi hiyo  ametembelea JKCI kwa lengo la kujitambulisha na kuzungumza na viongozi.
Katika mazungumzo hayo amewataka viongozi wa taasisi hiyo kuwa mfano na  kufanya kazi kwa bidii ili kuendana na kasi ya Rais John Magufuli  ya hapa kazi tu.
Pia amewapongeza kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuhakikisha watanzania wenye magonjwa ya Moyo wanapatiwa matibabu hapa hapa nchini hatua ambayo imepunguza gharama kubwa ya kugharamia matibabu nje ya nchi.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger