TRA

TRA

Monday, September 19, 2016

BREAKIN NEWZZ!!:- CHADEMA WAMFUKUZA KIGOGO WAO KWA UTAPELI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Freeman Mbowe, Mwenyekiti CHADEMA
Freeman Mbowe, Mwenyekiti CHADEMA 
By Pamela Chilongola,mwananchi
Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo( Chadema) wilaya ya Temeke kimemfukuza uanachama Diwani wa Kata ya Kurasini ambaye ni  mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa  Mivinjeni , Matiti Togocho
kwa kile walichodai kuwa amekuwa akifanya ufisadi ikiwemo kutengeneza hati za viwanja feki na kujipatia kipato.
 

Mwenyekiti Chadema wilaya hiyo Berdad Mwakyembe amesema wamefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha na makosa ya ufisadi aliyowafanyia wananchi wa kata yake.
 
Mwakyembe alisema diwani huyo ameshindwa kuwaletea maendeleo wananchi wake badala yake alikuwa anatumia nafasi yake kujinufaisha huku akiwawakandamiza wananchi wanyonge.
Hata hivyo Diwani Togocho alisema hatozungumzia suala hiko hadi atakapopewa ruhusa kutoka kwa mratibu wa kanda kuongea suala hilo
 
“Unajua aliyeongea mwenyekiti wangu hivyo siwezi kuropoka kitu hadi nisikilize mabosi wangu ambaye mratibu wa kanda,”alisema Togocho.
Source:- Mwananchi/Citizen

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger