TRA

TRA

Monday, September 5, 2016

CUF Watoa Waraka Kwa Rais Magufuli

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Mtatiro-640x336
Chama Cha Wananchi CUF leo kipitia mkutano wake na wanahabari kimejibu kauli zilizotolewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Dk. John Magufuli alizozitoa juzi na jana (tarehe 2-3/9/2016) katika mikutano ya hadhara aliyoifanya katika kisiwa cha Pemba, Uwanja wa Gombani na Unguja katika Uwanja wa Demokrasia (Kibandamaiti).
Soma taarifa yao hapa chini;
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Waheshimiwa wanahabari,
Awali napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru kwa kuitikia wito wetu, nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoendelea kuifanya ya kutupasha habari mbalimbali zinazohusiana na hali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ndani ya nchi yetu na nje ya mipaka yake. Lakini pia kuwapa pole kutokana na namna mnavyotekeleza majukumu yenu katika mazingira magumu ya hofu na vitisho vinavyofanywa na watendaji wa serikali ya awamu ya tano. Nitumie fursa hii pia kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza rasmi kuzungumza na vyombo vya habari toka BARAZA KUU LA UONGOZI CUF TAIFA liniamini na kunipa dhamana kubwa ya utendaji na usimamizi wa chama chetu kwa kuniteua kuwa MWENYEKITI WA KAMATI YA UONGOZI WA CHAMA CHETU CHA WANANCHI CUF TAIFA, tukisimamia majukumu yaliyopaswa kufanywa na Mwenyekiti wa Chama Taifa na Makamu Mwenyekiti Taifa. Naahidi nitatekeleza wajibu wangu kwa uaminifu mkubwa na weledi wa hali ya juu kwa madhumuni ya kuwaletea watanzania mabadiliko sahihi ya maendeleo ya kisiasa na kiuchumi wanayoyataka katika Taifa letu.
Waheshimiwa wanahabari,
Tumewaiteni na kuomba kuzungumza nanyi kwa lengo la kujibu kauli zilizotolewa na Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli alizozitoa juzi na jana (tarehe 2-3/9/2016) katika mikutano ya hadhara aliyoifanya katika kisiwa cha Pemba, uwanja wa Gombani na Unguja katika uwanja wa demokrasia (Kibandamaiti) na kupitia nyinyi tufikishe ujumbe wetu kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais JOHN MAGUFULI na watanzania kwa ujumla. Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli amezungumza mambo mengi na pia amejikita katika kutoa kauli za dhihaka na mipasho dhidi ya Chama cha Wananchi CUF na katibu mkuu wetu Maalim Seif Sharif Hamad jambo ambalo tunaamini kwa hadhi na heshima ya nafasi yake na hadhi ya taasisi ya urais hakupaswa kufanya hivyo kama kiongozi wa nchi. Pamoja na masuala mengine Mwenyekiti wa CCM, Rais JOHN MAGUFULI amesema amekwenda kuwashukuru wananchi wa Unguja na Pemba kwa kumchagua yeye pamoja na Dokta Ali Mohamed Shein, amewahahakishia Wazanzibari kuwa atailinda amani ya nchi kwa nguvu zake zote na yeyote atakayejaribu kuivuruga amani atamshughulikia kwa nguvu zake zote bila huruma, ataulinda Muungano kwa nguvu zake zote na lazima uendelee kudumu katika kipindi chote cha utawala wake. Tatu, amezungumzia maendeleo – Maji, viwanda, miundombinu, uvuvi na kadhalika lakini pia amezungumzia kuitunza amani akitolea mifano ya nchi zisizokuwa na amani ikiwemo Libya, Iraq, Syria, Somalia na mauaji ya kimbali yaliyotokea Rwanda mwaka 1994. Magufuli amepongeza aliyooiita “kazi nzuri ya majeshi” nadhani kwa kuisaidia kupata ushindi na kuwathibiti wanaotaka mabadiliko na amempongeza Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa ZEC, kwa kufuta uchaguzi wa tarehe 25/10/2016 uliompa ushindi Maalim Seif Sharif Hamad, na kumuombea apewe tuzo kwa kazi nzuri aliyoifanya. Anashangaa kwanini Dokta Shein ameunda serikali kwa kuvishirikisha vyama vingine wakati alishinda (Shein) kwa asilimia 99 huku akijigamba kuwa yeye kamwe hawezi kuingiza na hataingiza mtu hata mmoja kutoka upinzani katika serikali yake pamoja na kupata ushindi wa asilimia 58 anasahau kuwa hivi karibuni amemteua Mwenyekiti wa TLP Mhe. Agustino Lyatonga Mrema, kuwa Mwenyekiti wa bodi ya PAROLE.
MSIMAMO WA CUF JUU YA KAULI ALIZOZITOA RAIS MAGUFULI:
THE CIVIC UNITED FRONT (CUF CHAMA CHA WANANCHI) kimesikitishwa na kauli zisizofaa kwa heshima na hadhi ya taasisi ya urais na nafasi yake kama kiongozi wa nchi kutoka kauli za uchochezi, kupandikiza chuki na uhasama, kuwagawa wananchi na kutaka kujenga chama chake kwa njia ya vitisho na kutumia vyombo vya dola. Tunamtaka Mwenyekiti wa CCM, Rais Magufuli atambue kuwa hatoweza kujenga umoja wa watanzania kwa kutoa kauli za kuimarisha chuki, uhasama na kutosimamia haki, na kuunga mkono vitendo vya uvunjaji wa demokrasia na sheria za nchi. Rais Magufuli hawezi kuwa mfano wa kuigwa kwa vizazi vijavyo katika mikakati ya mataifa masikini ya kulinda sheria, haki za kiraia, utawala bora na kuleta maendeleo shirikishi (Inclusive Develeopment).Kauli nyingi za kuchochea chuki na uhasama alizozitoa Rais Magufuli si za kwanza wala si ngeni kwa Wazanzibari. Kisiasa wazanzibar na hasa wafuasi wa CUF (ambao ni wengi) wamekuwa waathirika wakubwa wa matumizi makubwa ya ukandamizaji na unyanyasaji iunaofanywa kikatili sana kupitia MAJESHI, MAZOMBI, JANJAWIDI nakadhalika. Mauaji yaliyofanywa na Serikali ya CCM chini ya utawala wa serikali ya awamu ya Tatu iliyoongozwa na Benjamini William Mkapa Januari 26-27, 2001
yalisababisha watu 46 kuuliwa na vyombo vya Ulinzi, watu 38 wameuwawa kwa kificho mpaka leo hawajaonekana. Watanzania 658 waliojeruhiwa, na 135 waliopata vilema vya kudumu katika maisha yao. Aidha zaidi ya wazanzibar 4000 waliishi kama wakimbizi Shimoni, Mombasa nchini Kenya, orodha yao tumeiambatanisha na taarifa hii. Kama kweli Rais Magufuli anataka kulinda amani ya Tanzania haiwezekani kuwa raia wamekuwa wakipigwa na kuteswa na kukatwa viungo vyao na kuporwa mali zao na vikosi vya majeshi, Mazombi na akiwa kimya na kutoa kauli za kubariki vitendo hivyo. Kwa mtizamo wa Magufuli, ukatili na uhuni unaotendwa na MAZOMBI ukiungwa mkono na vikosi vya majeshi ya SMZ na vile vya Muungano eti ndiyo ulinzi wa amani. Lakini, Kauli mfano wa hizi zimewahi kutolewa na watangulizi wake na viongozi wa Zanzibar waliopita. Hata hivyo mwisho wa yote hawakuweza kufanikiwa kuwahadaa wazanzibari kudai haki yao na mwaka hadi mwaka wazanzibar wanaotaka mabadiliko wawekuwa wakiongezeka na kuidhihirishia dunia kuwa hawawezi kuvunjwa moyo na vitisho, hujuma na ukandamizaji.
Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli amemsifia Dokta Ali Mohamed Shein kwa kuchaguliwa kuwa Rais wazanzibar kwa kura nyingi. Jambo hili linachekesha na kustaajabisha dunia, kwani Hata mtoto mdogo anayeishi Zanzibar au Tanganyika anatambua kuwa Dr. Shein si rais halali wa Zanzibar. Ni rais aliyeingizwa madarakani kwa kile kinachoweza kuitwa “tyranny of the highest order of the African Power Mongers who are ready to shed blood for power” yaani “udhalimu wa kiwango cha juu kabisa kinachofanywa na viongozi waroho wa madaraka ambao wako tayari kumwaga damu ili watawale”. Katika uchaguzi halali wa tarehe 25/10/2016. Wazanzibar walimchagua kwa kura nyingi kabisa, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa Rais wao. Wazanzibari wanajua hivyo, Watanzania wanajua hivyo, Waafrika wanajua hivyo na dunia inaimba wimbo huo. Kujidanganya kuwa Dokta Shein ni rais halali wa Zanzibar ni uotaji wa ndoto ya mchana kuwa Tanzania ina viwanda kila kata na kila kijiji, ndoto ambayo kwa aina ya uongozi wa John Magufuli haiwezi kutimia.(P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger