TRA

TRA

Monday, September 5, 2016

Naibu Waziri Mh. Chumu Kombo Khamis awataka vijana kuanzisha vikundi vya ujasiriamali

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



MH.CHUMU-K.KHAMIS
Na Masanja Mabula -Pemba
NAIBU waziri wa Habari , Utalii , Utamaduni na Michezo Bi Chumu Kombo Khamis amewataka vijana kujikusanya na kuanzisha vikundi vya uzalishaji mali ili waweze kujiletea maendeleo .
Amesema , zipo fursa nyingi ambazo zinaweza kuwakomboa vijana kutoka katika wimbi la umaskini iwapo watazitumia ipasavyo kwa kukaa pamoja na kubuni shuhuli za maendeleo .
Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na vijana wa Jimbo la Micheweni ambapo amebainisha fursa hizo kuwa ni sekta ya Michezo ambayo imekuwa ikitoa ajira kwa vijana .
Aidha Naibu Waziri amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Habari , Utalii , Utamaduni na Michezo itaendelea kuwaunga mkono vijana wenye nia ya kujiajiri kupitia sekta mbali mbali .
“Zipo fursa nyingi ambazo ikiwa zitatumika ipasavyo , suala la umaskini kwa vijana litakuwa ndoto , hivyo naomba mzitumie kwa ajili ya kupata ajira miongoni mwake ni sekta ya Michezo ” alisisitiza Naibu Waziri.
Mapema akizungumza katika hafla hiyo , Hamad Mbwana amewataka vijana kuacha kutegemea aajira kutoka serikalini badala yake wahakikishe wanazzitumia fursa zilizopo kutengeneza ajira zao binafsi.
Amesema zama za kutegemea ajira kutoka Serikalini kwa wakati huu zinaweza kumdumaza kijana , kutokana na serikali kutoa ajira kidogo kulingana na Idadi ya vijana waliosoma , hivyo fursa pekee ni kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali .
“Ni lazima tuelewe kwamba vijana waliosoma ni wengi hivyo hawawezi kuajiriwa wote na Serikali kwa wakati mmoja , hivyo fursa pekee ni kujiajiri wenyewe kupitia sekta mbali mbali ikiwemo michezo “alifahamisha .
Kwa upande wao , baadhi vijana wamesema kwamba bado zipo changamoto zinazowakabili ikiwemo suala la mitaji na kuiomba Serikali kusaidia kuwapatia taalauma ambayo wataitumia katika kufikia maendeleo waliyokusudia . (P.T)

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger