TRA

TRA

Saturday, October 22, 2016

WAANDSHI WA HABARI WAASWA KUELIMISHA UMMA KUHUSU MAGONJWA YASIYOPEWA KIPAUMBELE

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


 Ofisa Mradi wa Mpango wa Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele, Oscar Kaitaba akielezea umuhimu wa vyombo vya habari kuelimisha umma kujenga tabia ya  kutumia Kingatiba ya magonjwa ya kichocho, Minyoo ya Tumbo, Usubi Matende na Mabusha wakati wa Warsha iliyoshirikisha wanahabari, Dar es Salaam leo. Kampeni ya kuwapatia wananchi Tibakinga kwa wakazi takribani mil. 4 wa Jiji la Dar es Salaam itaanza Oktoba 25 waka huu. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
 Meneja Mradi wa Mpango wa Magonjwa Yaliyokuwa Hayapewi Kipaumbele, Upendo Mwingira akifafanua jambo wakati wa warsha hiyo.
 Wanahabari wakiwa katika warsha hiyo
 Mtangazaji wa BBC, Halima Kassim akitafakari jambo  kuhusu semina hiyo ya wanahabari kupata uelewa kuhusu magonjwa hayo na jinsi ya kuwaelimisha wananchi kutumia Kingatiba kwa kumeza  dawa mara noja kila mwaka ili kuboresha afya
 Mtaalamu Kaitaba akionesha baadhi ya dawa za Kingatiba ya magonjwa hayo
 Ofisa Habari wa Mradi huo, Said Makora akiwataka wanahabari kuwaelimiasha wananchi juu ya magonjwa hayo na jinsi ya kupata Kingatiba kwa kuandika makala, habari, majarida na kutumia mitandao ya kijamii kwa nia ya kuyatokomeza magonjwa hayo kufikia mwaka 2020.
 Kaitaba akionesha vifaa vinavyotumika kuwapima watu ili wapewe dawa kulingana na kimo chake.
 Mwandishi wa Habari wa Nipashe, Jasmin akichangia mada wakati wa semina hiyo.
 Wana habari wakipatiwa dawa za Kingatiba za magonjwa hayo
Mtangazaji wa E FM Radio akipimwa urefu ndipo apatiwe dawa 

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger