Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Ashatu Kijaji akihutubia katika mkutano
wa tano wa mwaka wa ESRF wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake
kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania ulioandaliwa na Taasisi ya
Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.(Picha na Said
Khalfan wa KVS Blog)
"Serikali
inapofanya mipango inatakiwa kupanga mipango ambayo inajaribu kujibu
kero za mwananchi, kama ni elimu, kama ni afyaa au kama ni kilimo cha
kisasa, tunapotengeneza sera tuwe tunauwianisha, hizo sera
zikitekelezeka na mteja wa bidhaa awe ameandaliwa ili mkulima asiwe
amepoteza nguvu bure," alisema Luhanjo na kuongeza.
"Tunazungumzia
nchi ya viwanda, viwanda gani? na nchi yetu niya kilimo kwahiyo
tunatarajia viwanda vingi vitakuwa ni vya kilimo, kwahiyo tunataraji
mkulima mdogo aimalishwe ili aweze kuzalisha mazao yanayokwenda
kiwandani ni lazima sera ziwe na uwiano mzuri."
Nae Naibu
Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji alisema
Serikali inafahamu kuwa nchi haiwezi kupiga hatua bila kuhusisha
mwananchi mmoja mmoja na inachofanya kwa sasa na kuwashawishi watu wenye
viwanda kutumia malighafi ambazo zinazalishwa nchini ili wakulima
nchini wafaidike na uwepo wa viwanda nchini.
"Tunaamini
hatuwezi kuwa na uchumi unaokua kama hali ya kijamii ya wananchi haikui
na hata Rais Magufuli alikuwa akisema tangu akiwa katika kampeni kwamba
Tanzania ya Magufuli niya viwanda, na viwanda hivi ni kwa ajili ya watu
wetu,
Mwenyekiti
wa Bodi ya wadhamini wa ESRF, Philemon Luhanjo, akizungumza katika
mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake
kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania ulioandaliwa na ESRF.
"Kwenye
mpango wetu wa miaka mitano tumesisitiza maendeleo ya viwanda lakini
vinavyotumia malighafi zinazozalishwa hapa nchini katika kilimo chetu,
kwahiyo hatuwezi kuwa na viwanda kama kilimo hakijaendelea, hatuwezi
kuwa maendelo ya kijamii kama kilimo chetu hakijaendelea, kilimo ndiyo
uti wa mgongo wa taifa letu, kwahiyo tumejadili hilo ili kuona wananchi
wetu wananufaika vipi," alisema Kijaji.
Kwa
upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida alizungumza kuhusu
mkutano huo ambao umedhaminiwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa
Mataifa (UNDP) na kusema,"ESRF kwasasa hivi tupo kwenye mchakato wa
kutengeneza Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya mwaka 2017, "Katika hiyo
ripoti tumeweza kutaharisha ripoti 11 ambazo zitachangia katika
utayarishishaji wa hiyo ripoti na dhumuni kubwa ni kuweza kuzijadili
hizo ripoti na kupata uelewa mpana ni kwa kiasi gani sera za kijamii
zina mchango mkubwa katika kuleta mageuzi ya kiuchumi hapa Tanzania."
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi
Kida akitoa maelezo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika mkutano
huo.
Mkuu wa
Programu, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP, Amon Manyama
akizungumza katika mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na
mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania.(P.T)
SHARE
No comments:
Post a Comment