TRA

TRA

Friday, March 31, 2017

Wanawake, vijana tegemeo katika kumaliza machafuko nchini Somalia

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Mane Ahmed, Ofisa Jinsia kutoka African Union Mission in Somalia (AMISOM) akizungumza na waandishi.

Washiriki wa mkutano wakifuatilia mada zilizowasilishwa.


Wanawake na vijana ni nyenzo muhimu katika uhamasishaji wa kumaliza machafuko yanayoendelea nchini Somalia, wakati kundi hilo pia likilengwa zaidi na vikundi vya kigaidi kutumika katika matukio ya kigaidi.

Hayo yamebainishwa na Mane Ahmed, Afisa Jinsia kutoka African Union Mission in Somalia (AMISOM), wakati wa mkutano wa siku tatu unaomalizika leo (Ijumaa) jijini Dar es Salaam jana.

Mkutano huo ulioandaliwa na AMISOM kwa ushirikiano na serikali ya Somalia unalenga kutafuta njia stahiki za kuzuia vijana kudahiliwa na vikundi vya kigaidi nchini humo.

Pamoja na mambo mengine, mkutano huo umebainisha umuhimu wa ujengaji uwezo kama hatua madhubuti katika kueneza hali ya kuvumiliana ndani ya jamii na kuwapa sifa mbaya Al-Shabaab.

Akizungumza mkutanoni hapo, Bi Mane amesema kuwa Serikali ya Somalia imeanzisha ofisi ijulikanayo kama Counter-Violent Extremism (CVE) ikiwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kukamilisha rasimu ya kwanza ya Sera ya Kuzuia na Kupambana na Vikundi vyenye msimamo mkali.

Bi Mane alisema kuwa AMISOM imeanzisha Mtandao wa Kijinsia ambao umelenga katika kuzuia na kupambana na vikundi vyenye msimamo mkali kwa lengo la kusaidia juhudi za Shirikisho katika kuunganisha mtazamo wa kijinsia katika mpango na mikakati yake.

Bi Muna alisema: "Mkutano huu utawajengea uwezo viongozi wa dini, watendaji wa Somalia na kuongeza ufahamu wao juu ya umuhimu wa kuwajumuisha wanawake katika njia yao za kupambana na siasa kali na kubadilishana uzoefu na mbinu bora na wataalamu, watafiti, watendaji kutoka barani ambao wana ufanisi mkubwa katika kukabiliana na masuala yahusuyo vikundi vyenye misimamo mikali."

Aidha naye, Naibu Kamishna wa Polisi wa AMISOM, Christine Alalo alisema kuwa katika hatua hii muhimu ya safari ya Somalia kuelekea kwenye amani na utulivu, jukumu la wanawake, wanaume na vijana katika kukabiliana na vikundi vyenye msimamo mkali ni muhimu kutiliwa mkazo kwa kiasi kikubwa.

"Siyo siri kwamba wakati wa miongo miwili na nusu ya vita, wanawake na vijana wadogo wamekuwa wakitumika na makundi ya kigaidi katika Nyanja mbalimbali ikiwemo kukusanya taarifa za kiusalama, na kubeba mabomu,” alisema.

Alibainisha kuwa AMISOM wamefanya mengi katika kupambana na hilo kupitia kitengo cha jinsia, wanawake na ulinzi wa mtoto.

Alisema kuwa AMISOM pia imesaidia wizara ya wanawake, jinsia na haki za binadamu katika kuandaa sera ya taifa ya jinsia, kwa kufanya mafunzo ya ujengaji uwezo kwa wanawake wa Somalia na viongozi wa dini katika kumaliza mambo hatarishi.

Mkutano huo wa siku tatu ambao unamalizika leo jijini Dar es Salaam, umewaleta pamoja watendaji, viongozi wa dini na asasi za kijamii kutoka nchi nane (Somalia, Tanzania, Ethiopia, Nigeria, Kenya, Mali, Djibouti, Alger) ukijadili juu ya mada zinazohusiana na kukabiliana na siasa kali na ugaidi.

Jumla ya viongozi hamsini, wa kidini; watafiti na watendaji, na wadau muhimu kutoka taasisi za kitaifa, kikanda na kimataifa wameshiriki katika mkutano huo.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger