TRA

TRA

Friday, April 21, 2017

Ahmadinejad azuiliwa kugombea tena urais wa Iran

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Baraza la uangalizi nchini Iran limemzuia rais wa zamani wa nchi hiyo Mahmoud Ahmadinejad kuwa mgombea katika uchaguzi wa rais utakaofanyika mwezi ujao.
 
 Ahmadinejad mwenye misimamo mikali aliwashtusha wairan wiki iliyopita, alipotangaza nia yake ya kuingia tena katika kinyang'anyiro cha urais. 
 
                     Mahmoud Ahmadinejad
 
Kituo cha televisheni ya taifa ya Iran kimesema baraza lenye jukumu la kuchunguza majina ya wagombea, limeliondoa jina lake katika orodha ya watakaowania wadhifa huo.
 
 Rais wa sasa Hassan Rouhani ni mmoja wa wagombea sita ambao wameridhiwa na baraza hilo.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger