TRA

TRA

Saturday, April 29, 2017

Duterte: kusini mashariki mwa Asia kuna tishio la madawa haramu

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Rais wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, leo amewaonya viongozi wa Asia ya Kusini-Mashariki kwamba wanakabiliwa na tishio kubwa la madawa haramu linaloweza kuharibu jamii zao, huku akitoa wito wa ushirikiano wa pamoja.


                          Rodrigo Duterte

Duterte anayelaaniwa na jumuiya ya kimataifa kwa operesheni yake ya ukandamizaji ya kupambana na madawa la kulevya iliyosababisha vifo vya maelfu ya watu, pia amesisitiza kwamba watu wa nje wasiingilie mambo ya ndani ya Asia ya Kusini-Mashariki. 

Katika hotuba yake kwa viongozi waliohudhuria Mkutano wa kilele wa ASEAN wa nchi za kusini mashariki mwa Asia, Duterte alizungumzia mila ya eneo hilo ya kutotaka kuingiliwa katika mambo yake. 

Kiongozi huyo wa Ufulipino aligusia pia mahusiano na Marekani pamoja na Umoja wa Ulaya, ambao wamekuwa wakionyesha wasiwasi juu ya mauaji ya kiholela yanayofanyika katika vita vyake dhidi ya madawa ya kulevya.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger