Staa wa Bongo Movie, Salim Ahmed ‘Gambo’.
KUFUATIA
uwepo wa madai kuwa amelionja penzi la mwigizaji Wema Sepetu, mkali
anayekimbiza kwa sasa katika soko la sinema kwa Bongo, Salim Ahmed
‘Gambo’ amebanwa na Risasi na kufungukia uhusiano wao.
Wema na Gabo.
Awali,
mwanahabari wetu alihakikishiwa na msanii mmoja (jina tunalihifadhi)
kuwa kabla ya kuvuja kwa picha za sinema za Wema na Gabo za filamu hivi
karibuni, wawili hao waliwahi kuanguka dhambini miaka kadhaa iliyopita.
“Kwani
unafiri ukaribu wa Wema na Gabo ni filamu tu? Kuna zaidi ya filamu,
walishawahi kutoka miaka ya nyuma na ndio maana umeona hivi karibuni
imekuwa rahisi tu kwao kufanya tena kazi pamoja,” alisema msanii huyo.
Baada
ya kupata ubuyu huo, mwanahabari wetu alimtafuta Wema ili kuweza
kumsikia anazungumziaje ishu hiyoi lakini bahati mbaya mrembo huyo
hakuweza kupokea simu na hata alipotumiwa ujumbe mfupi, pia hakujibu.
Alipoulizwa Gabo kuhusiana na madai hayo, alisema ukaribu wake na Wema
umekuwa ukitafsiriwa tofauti lakini ukweli ni kwamba yeye wanakutanisha
zaidi na kazi tu na si vinginevyo.
“Mimi
si mara moja au mara mbili. Wema nakutana naye, nakuwa karibu naye kwa
ajiuli ya kazi. Umeona picha mpya za kimahaba hivi karibuni, zile ni za
muvi tu,” alisema Gabo.
SHARE
No comments:
Post a Comment