TRA

TRA

Saturday, April 22, 2017

MENEJA WA MSHAMBULIAJI KINDA WA SIMBA ALIA NA KOCHA OMOG

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !




Meneja wa kiungo mshambualiaji wa Simba, Hija Uganda amelalama kwamba kitendo cha Kocha Joseph Omog kutompa nafasi ya kucheza mchezaji wake ni kuua kipaji chake.


Meneja wa Ugando, Jamali Kisongo amesema kuwa kitendo cha mchezaji huyo kukosa nafasi ya kucheza chini ya Omog, kimekuwa hakimfurahishi ndipo alipoamua kuchukua uamuzi huo wa kutaka aondoke zake klabu hapo ili akatafute maisha sehemu nyingine ambako atakuwa akipata nafasi ya kucheza mara kwa mara.

“Kwa mchezaji anayejitambua hata siku moja hafurahii kukaa benchi bila ya kucheza, Ugando kwa sasa maisha yake ndani ya Simba siyo mazuri hapati nafasi ya kucheza jambo ambalo linaweza kuua kipaji chake.


“Kutokana na hali hiyo, hivi sasa nipo katika mazungumzo na uongozi wa Simba ili baada ya msimu huu uweze kumuachia akatafute maisha sehemu nyingine ambako atapata nafasi ya kucheza ili aweze kuinua kipaji chake,” alisema Kisongo.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger