Waziri Jenista Mhagama akiwa na
Naibu Wake Anthony Mavunde katika ukaguzi wa shamba lenye ukubwa wa
ekari 6000 ambalo ni mahsusi kwa ajili ya Ufugaji wa Ng’ombe na Mbuzi
Wami Sokoine Mvomero leo tarehe 23.04.2017.
Katika eneo hilo pia kutakuwa machinjio ya mifugo na kiwanda
cha kuchakata nyama ambacho kinatarajiwa kutoa Ajira zaidi ya 3000 za
moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja.Pamoja na kiwanda hicho,pia kutakuwa na chuo cha mafunzo ya uchakataji wa ngozi na utengenezaji wa bidhaa zitokanazo na ngozi.
Wafugaji watapata soko la uhakika la mifugo yao na hivyo kutatua changamoto ya ukosefu wa masoko ya uhakika kwa wafugaji hasa katika Mkoa wa Morogoro na nchi nzima pia,jumla ya Ng’ombe 300 watachinjwa kila siku.
SHARE
No comments:
Post a Comment