Jaji mmoja nchini India ambaye amekuwa mafichoni tangu ahukumiwe kifungo jela amekamatwa na kufungwa.
Alikamatwa katika jimbo la kusini la India Tamil Nadu siku ya Jumanne usiku.
Alihukumiwa kifungo mjini Kolkata huku ombi lake la kumwachilia kwa dhamana siku ya Jumatano likikataliwa na mahakama ya juu zaidi.
Jaji huyo wa zamani alipatikana na hatia ya kutoa madai dhidi ya majaji wenzake.
Alihukumiwa kwa kukaidi agozi la mahakama na mahakama ya juu zaidi baada ya kutuma barua kwa waziri mkuu Narendra Modi ambapo alimtaka kuwachukulia hatua majaji wenzake.
Alipokonywa nguvu zake kama jaji mnamo Februari. BBC
SHARE
No comments:
Post a Comment