TRA

TRA

Wednesday, June 7, 2017

Korea Kaskazini yarusha kombora la kushambulia meli

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !



Korea kaskazini imerusha makombora kadha ya kushambulia meli mashariki mwa pwani kwa mujibu wa Korea Kusini.

Mamlaka zilisema kwa makombora hayo yaliyorushwa Alhamisi asubuhi karibu na mji wa Wonsan yalikuwa ni ya masafa mafupi.
Makombora hayo yaliruka umbali wa kilomita 200 kabla ya kuanguka baharini.

 Marekani inaweka mitambo ya kujikinga nchini Korea Kusini
Majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini mwaka huu yamekiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
Wataalamu wana hofu kuwa majaribio hayo na hatua za Korea kutundika silaha za nuklia katika vichwa vya makombora. 

Msemaji wa Jeshi la Korea Kusini amesema kuw majiribio ya hivi punde yalionyesha kuwa Korea Kaskazini ilitaka kuonyesha kuwa ina uwezo wa kulenga meli kubwa baada ya mazoezi ya hivi majuzi kati ya Marekani na vikosi vya Korea Kusini.
 Korea Kaskazini ikionyesha makombora ya Styx 2012
Makomboa ya kushambulia meli ni makombora ambayo huelekezwa. Mwaka 2012 Korea Kaskazini ilionyesha makomboa kadha kama hayo yanayojulikana kama Styx.

Lakini hapo awali Korea ilijaribu bila mafanikio kufanyia majaribio makombora ya kushambulia meli.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger