Mwandishi Wetu
RAIS John Magufuli ameanza ziara mkoani Pwani leo na kusisitiza kuwa wezi watamkoma.
Alisema wapo baadhi ya matapeli walikuwa wananyonya Watanzania kwenye uwekezaji wa umeme huku akibainisha kuwa anachukia wezi na hakuna atakayepona.
"Nachukia wezi, wezi watakoma tu. Awe anatoka Ulaya, Tanzania mwizi ni mwizi tu lazima wale wa chuya," alisema.
Pia alisema serikali imeziba mianya iliyokuwa inapoteza fedha, ikiwemo bandarini kutokana ukusanyaji wa kodi.
Magufuli alisema waliokuwa wanafuja fedha wameshughuliwa na wengine wapo mahakamani. "Fedha za kodi ndizo tunatumia kwenye elimu bure. Tumeanza kulipa madeni ya walimu na wakandarasi," alisema.
Alisema wameanza kulipa madeni ikiwemo ya walimu na kusisitiza kuwa wenye madeni halali watalipwa.
SHARE
No comments:
Post a Comment