Gavana wa jimbo la
Kivu ya Kaskazini Julien Paluku amesema zaidi ya wafungwa 900 wametoroka
baada ya kutokea shambulizi na kuvunja gereza moja huko Congo DRC.
Rais Joseph Kabila
Haijajulikana ni nani haswa aliyefanya shambulizi hilo.
Mwanaharakati mmoja anasema kwa makundi mengi yaliyojihami yanayojulikana kama Mai-Mai yanaendesha shughuli zao eneo hilo.
Siku ya Jumamosi wafungwa kadhaa walitoroshwa na mtu mmoja aliyekuwa na silaha.
Mwezi uliopita mamia ya wafungwa walitoroka katika jela moja kubwa mjini Kinshasa baada ya mtu mmoja aliyekuwa na silaha kuvamia jela hiyo usiku wa manane.
CHANZO: BBC
SHARE
No comments:
Post a Comment