TRA

TRA

Sunday, June 11, 2017

Mamia ya wafungwa watoroka gerezani DRC

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Gavana wa jimbo la Kivu ya Kaskazini Julien Paluku amesema zaidi ya wafungwa 900 wametoroka baada ya kutokea shambulizi na kuvunja gereza moja huko Congo DRC.

Watu 11 wameuawa katika tukio hilo Kaskazini Mashariki mwa mji wa Beni.


  Rais Joseph Kabila

Haijajulikana ni nani haswa aliyefanya shambulizi hilo.
Mwanaharakati mmoja anasema kwa makundi mengi yaliyojihami yanayojulikana kama Mai-Mai yanaendesha shughuli zao eneo hilo.
Siku ya Jumamosi wafungwa kadhaa walitoroshwa na mtu mmoja aliyekuwa na silaha.

Mwezi uliopita mamia ya wafungwa walitoroka katika jela moja kubwa mjini Kinshasa baada ya mtu mmoja aliyekuwa na silaha kuvamia jela hiyo usiku wa manane.

CHANZO: BBC

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger