TRA

TRA

Wednesday, June 21, 2017

MKUU WA WILAYA YA UBUNGO KISARE MAKORI AFUNGUA MAFUNZO KWA WENYEVITI, NA WATENDAJI KATA NA MITAA

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !


Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akizungumza wakati wa kufungua mafunzo kwa Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Manispaa ya Ubungo 
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akielezea lengo la mafunzo muda mchache kabla ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori kufungua mafunzo ya kuwajengea uwezo Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Manispaa ya Ubungo
Wakuu wa Idara na Vitengo Manispaa ya Ubungo sambamba na Wenyeviti wa Mitaa na Watendaji wa Kata na Mitaa wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori wakati wa kufungua mafunzo ya siku nne ya kuwajenega uwezo Wenyeviti wa Mitaa na Watendaji wa Kata na Mitaakwa.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg Jmaes Mkumbo akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori kufungua mafunzo kwa Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Manispaa ya Ubungo
Mkuu wa Idara ya Mipango na Uchumi Manispaa ya Ubungo Ndg Yamo Wambura (Kulia) sambamba na Hosia Kivulenge wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori wakati akifungua mafunzo kwa Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Manispaa ya Ubungo
Afisa Utumishi Mkuu wa Manispaa ya Ubungo Ndg Ally Juma Ally akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori wakati akifungua mafunzo kwa Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Manispaa ya Ubungo
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akizungumza wakati wa kufungua mafunzo kwa Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Manispaa ya Ubungo
Wakuu wa Idara na Vitengo Manispaa ya Ubungo sambamba na Wenyeviti wa Mitaa na Watendaji wa Kata na Mitaa wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori wakati wa kufungua mafunzo ya siku nne ya kuwajenega uwezo Wenyeviti wa Mitaa na Watendaji wa Kata na Mitaakwa.
Baadhi ya Watendaji wa Kata wakishangilia jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akielezea lengo la mafunzo muda mchache kabla ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori kufungua mafunzo ya kuwajengea uwezo Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Manispaa ya Ubungo
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akifatilia kikao kabla ya kufungua mafunzo kwa Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa Manispaa ya Ubungo
 
Na Mathias Canal, Dar es salaam
 
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori leo June
21, 2017 amefungua mafunzo ya kuwajengea uwezo 
Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa yatakayofanyika kwa siku nne katika ukumbi wa
Manispaa ya Ubungo kuhusu Mwongozo mpya wa mapokezi na Matumizi ya fedha za
LGDG (Local Government Development Grant), Mpango wa fursa na vikwazo kwa
maendeleo (O and OD-Oportunity and Obstacle to Development), Rushwa mahala Pa
kazi, Ulinzi na Usalama, Na sheria ya Ardhi.
 
Mafunzo hayo pia yatahusisha masuala ya Utawala
bora, Majukumu ya Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji wa Kata na Mitaa, Pia kujifunza
kuhusu historia na uhalali wa serikali za Mitaa, Sheria za uendeshaji wa
Mamlaka za serikali za Mitaa, Muundo, Madaraka na Majukumu ya serikali za
Mitaa, Mamlaka za serikali za Mitaa, Maadili ya viongozi wa Umma na Ulinzi na
usalama katika maeneo ya kazi.
 
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mhe
Makori alisema kuwa mafunzo hayo yanayotolewa ni sehemu ya utekelezaji wa
mpango wa mafunzo ulioidhinishwa na Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo kwa mwaka
wa fedha 2016/2017.
 
Alimpongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg
John Lipesi Kayombo kwa kuandaa mafunzo hayo kwani yatatoa fursa kwa Wenyeviti
na Watendaji wa Kata na Mitaa kuimarika katika nidhamu ya utendaji hususani
kutekeleza mambo yaliyoainishwa kutekelezwa katika maeneo yao kwa maslahi ya
wananchi.
 
Alisema kuwa mafunzo hayo yatatoa ufanisi wa uelewa
mipaka na mamlaka katika utendaji jambo ambalo litawasaidia kuepuka migongano
ya kimaslahi katika utekelezaji wa shughuli za uwakilishi wa wananchi pamoja na
kusimamia utekelezaji wa shughuli za Halmashauri.
 
Aliongeza kuwa mada zote ziatakazotolewa itakuwa ni
chachu ya kufungua ukurasa mpya kwa kuzingatia misingi ya utawala bora kwa
kufuata miiko ya uongozi na kuongeza uadilifu katika utendaji kazi wa kila siku
ili kufikia malengo yaliyoidhinishwa.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg
John Lipesi Kayombo alisema kuwa lengo la mafunzo hayo yanayotolewa kwa
Wenyeviti wa Mitaa, Watendaji Kata na Mitaa katika Manispaa ya Ubungo ni
kuwajengea uwezo katika kutatua matatizo ya wananchi, kuwasilisha mawazo yao
katika vikao vya kisheria, kuchambua sera na mikakati ya kutekeleza mipango
mbalimbali, kutafuta ufumbuzi wa changamoto za wananchi katika maeneo yetu ya
kusimamia majukumu yetu kikamilifu.
 
MD Kayombo alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga
kuinua kiwango cha utendaji kazi kwa kuongeza stadi na maarifa ya uongozi
ambayo yatachangia kuongeza tija na ufanisi katika shughuli zao ikiwa ni pamoja
na kuondoa migogoro ya kila siku baina ya Wenyeviti wa Mitaa na Watendaji wa
Kata na Mitaa.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger