TRA

TRA

Friday, June 30, 2017

Ndege ya Rais wa Nigeria yaegeshwa kwa siku 50 London

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Ofisi ya Rais nchini Nigeria imekiri kuwa ndege rasmi ya Rais Muhammadu Buhari imeegeshwa kwa zaidi ya siku 50 kwenye uwanja wa ndege mjini London.

Rais Buhari ambaye ni mgonjwa aliondoka nchini Nigeria kwa likizo ya kimatibabu tarehe 7 mwezi Mei akiitumia ndege hiyo.

 Rais Muhammadu Buhari (kushoto) na makamu wake Yemi Osinbajo

Ofisi ya Rais ilikuwa ikijibu ripoti za mitandao ya kijamii ambapo baadhi ya watu nchini Nigeria, wameelezea ghadhabu yao kutokana na kuegeshea ndegr hiyo mjini London.
Ilidaiwa kuwa ndege hiyo inalipigwa pauni 4000 kwa siku kama ada ya kuiegesha, katika uwanja wa Stansted mjini London, na kwa muda wa siku 50 imegharimu nchi hiyo pauni 200,000.

Msemaji wa Rais, Garba Shehu, alikana kuwa nchi inalipa pesa nyingi kwa nafasi hiyo. Aliiambia BBC kuwa gharama ya kuegesha ndege hiyo haitazidi pauni 1000.

Rais  Buhari amekuwa nje ya nchi kwa karibu miezi miwili kupata matibabu mjini London.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger