TRA

TRA

Friday, June 30, 2017

Ujerumani yaichapa Mexico 4-1 kombe la mabara

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

Iliwachukua Mexico dakika 89 kuweza kumfunga Marc-Andre ter Stegen

 

Ujerumani imefanikiwa kutinga fainali ya michuano ya kombe la mabara baada ya kuichapa bila huruma Mexico 4-1.

Leon Goretzka alifunga mara mbili katika mtanange huo katika dakika ya 6 na 8.

Magoli mengine ya Ujerumani yaliwekwa kimiani na Timo Werner dakika ya 59 na Amin Younes dakika ya 90.






Goli la kufutia machozi kwa upande wa Mexico lilipachikwa na Marco Fabian dakika ya 89.

Mexico walipata nafasi nyingi lakini hawakuweza kuzitumia vyema huku Ujerumani ikionekana kukomaa vilivyo katika safu ya ulinzi.

Fainali ya kombe la mabara itapigwa jumapili ya Julai 2 mbili kati ya Ujerumani na Chile mjini St Petersburg, huku mchezo wa awali ukizikutanisha Ureno na Mexico kutafuta mshindi wa tatu.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger