NA K-VIS BLOG/Mashirika ya Habari
SAIF
al-Islam, mtoto wa aliyekuwa kiongozi wa Libya, marehemu Muamar Gaddafi
ameachiwa kutoka gerezani chini ya sheria mpya ya msamaha.
Kuachiwa
kwake kumethibitishwa na moja ya utawala wa Libya wenye makazi yake kwenye mji
wa Mashariki wa Tobruk.
Mahakama
ya Tripoli ilimuhukumu al-Islam adhabu ya kifo mnamo mwaka 2015 kutokana na
makosa ya jinai vitani (war crimes) na kukandamiza wandamanaji wakati wa uasi
wa mwaka 2011 dhidi ya utawala wa baba yake.
Kwa
mujibu wa taarifa ya wapiganaji waliokuwa wanadhibiti gereza alilokuwa
akishikiliwa al-Islam kwenye kwenye mtandao wa Facebook, na kiongozi wa
wapiganaji hao, Abu Bakar al-Saddiq, al-Islam aliachiwa tangu Jumamosi.
Taarifa
hiyo ilisema, wameamua kumuachia al-Islam baada ya maombi ya Baraza la
Wawakilishi (HoR), bunge lenye makazi yake kwenye mji wa Tobruk.
Mtoto
huyo wa Gaddafi, pia anatakwia na mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai,
(ICC).
SHARE
No comments:
Post a Comment