Msajili
wa Hazina nchini, Dk Osward Mashindano (kushoto) akikata utepe ikiwa ni
ishara ya uzinduzi wa Jengo la Ofisi mpya ya Benki ya TPB. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu TPB, Sabasaba Moshingi ,ambapo ofisi hiyo mpya ipo
katika eneo la Mwanjelwa jijini Mbeya.
Msajili wa Hazina Nchini Dkt ,Osward Mashindano akizindua jiwe la msingi katika benki ya TPB iliyopo eneo la Mwanjelwa.
Msajili
wa Hazina Nchini Dkt ,Osward Mashindanoakizungumza katika hafla ya
uzinduzi wa jengo jipya la ofisi ya benki ya TPB Mwanjelwa.
Afisa
Mtendaji Mkuu TPB SabaSaba Moshingi ,kushoto akimkabidhi ripoti ya Mwaka
Msajili wa Hazina Dkt Osward Mashindano katika hafla ya uzinduzi wa
ofisi mpya ya jengo la Tpb Mwanjelwa jijini Mbeya.
Msajili
wa Hazina Nchini Dkt ,Osward Mashindano akionesha kadi maalum
aliyokabidhiwa na benki ya TPB mara baada ya kuzindua jengo hilo la
ofisi eneo la mwanjelwa jijini Mbeya.
Meza kuu katika picha ya Pamoja na wafanyakazi wa TPB.
TAASISI za kifedha nchini, zimetakiwa kuboresha mifumo ya utendaji kazi, ili kwenda sambamba na mabadiliko ya ukuaji wa uchumi.
Kauli
hiyo, ilitolewa jana na Msajili wa Hazina Dkt .Osward Mashindano, wakati
akizindua Ofisi kuu ya Benki ya TPB iliyoko katika eneo la Mwanjelwa
Jijini Mbeya.Amesema, wakati uchumi wa dunia unakua ni vema taasisi hizo
zikajiimarisha kiutendaji ili kukidhi vigezo vya ushindani wa
kibiashara ndani na nje ya nchi.
“Serikali
imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha sekta za kifedha nchini
zinatoa msukumo unaotakiwa kwenye shughuli za kiuchumi, hivyo ni wakati
wenu nanyi kubadili mifumo ya utendaji kazi ili kwenda sambamba na
ukuaji huo wa uchumi“,alisema.
Aidha
ametoa wito kwa taasisi za kifedha nchini kuhakikisha inaweka mazingira
rafiki kwa wananchi wa kipato cha chini kwa kuweka gharama nafuu za
huduma zao ili waweze kuzimudu.Pia, Mashindano ameipongeza benki ya TPB
kutokana na na jitihada zake za kupeleka huduma karibu na wananchi kwa
kutumia teknolojia ya kisasa na mawakala.
Hata
hivyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPB, Sabasaba Moshingi, alisema benki hiyo
imetoa gawio kwa serikali kiasi cha shilingi Bilioni 1.2 ambapo hundi
hiyo inatarajiwa kukabidhiwa mjini Dodoma.
SHARE
No comments:
Post a Comment