TRA

TRA

Sunday, June 11, 2017

TTB kwenda kuvitangaza vivutio vya utalii Israel

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !

NA MWANDISHI WETU 

BODI ya Utalii Tanzania (TTB) inafanya ziara ya siku tatu nchini Israel kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini hasa wanyamapori wanaopedwana raia wa nchi hiyo.
 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa TTB, Devota Mdachi alisema ziara hiyo itakayoanza Juni 11 hadi 15 mwaka huu itawasaidia kukutana na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii ikiwemo vyombo vya habari na wawekezaji.
 
“Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii pia atakuwa sehemu ya ziara hii, ambapo tutakutana na wadau zaidi ya 100 wa utalii pamoja na mawakala wa utalii tutakaowashawishi watuletee watalii wengi zaidi.
 
“Takwimu zinaonyesha kila mwaka watalii kutoka Israel wanaongezeka, kwa mfanoo mwaka 2011 walikuja watalii 3000 kutoka Israel na mwaka 2016 walikuja 15,000 ni 0ngezeko la zaidi ya mara tano ndani ya miaka minne,” alisema Bi. Devota.
 
Aliweka wazi kuwa watakapokutana na wenyeji wao Bodi ya Utalii Israel watakuwa na mazungumzo ya kina kuhusiana na kubadilishana uzoefu katika sekta hii muhimu kwa maendeleo ya nchi pamoja na kujua mbinu wanazotumia kupata watalii wengi.
 
“Tunajua Israel ni taifa la kiroho, historia yake inajipambanua kuwavutia watua wengi kuitembelea, lakini hata sisi nchini kwetu kuna maeneo mengi ya kihistoria tutahakikisha tunayatangaza kadiri tutakavyoweza, kwa sababu sehemu ya ziara yetu tutazungumza katika redio mbalimbali za nchi hiyo ikiwemo redio ya taifa inayosikika Israel nzima.
 
 
 
Mkurugenzi wa Bodi ya Taifa ya Utalii (TTB) Bi. Devotha Mdachi(kulia) akimwelekeza Balozi wa ukarimu 'Goodwill Ambassador' wa TTB Irene Veda sehemu za kusaini mkataba wake wa miaka miwili hivi karibuni.
 
“Hivi tunavyozungumza tayari matangazo katika redio yanaendelea kuwa kuna ujumbe unatoka Tanzania kuja kutangaza vivutio vya utalii, Waisrael kila mwaka wanakuja kuangalia mbuga za wanyama tunajua wanapenda sana wanyamapori,” alisema Bi. Devota.
 
Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo wa TTB alibainisha kuwa katika ziara yao watakuwa na siku moja ya kukutana na wawekezaji upande wa malazi, yaani hoteli. 
 
Ambao watawashawishi waje kuwekeza nchini ili ongezeko la watalii liendane na malazi bora yenye hadhi ya kimataifa.
Tanzania ni miongoni mwa mataifa yanayoongoza kuwa na vivutio vingi vya kitalii, inakadiriwa zaidi ya asilimia 38 ya ardhi yake imehifdhiwa kwa ajili ya utalii. 
 
 
Vilevile sekta hii inachangia asilimia 13 ya pato la taifa, mwaka 2013 iliingizia taifa pato la Dola za Kimarekani bilioni 4.48 zawa na zaidi ya Sh trilioni tisa.
Mwisho

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger