BANK
OF AFRICA hii leo imekabidhi rasmi mtambo wa ujenzi (Greda jipya aina
ya JCB) lenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 300 kwa kampuni ya
Dezo Civil Contactors Limited, kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali
ya ujenzi ikiwemo kandarasi ya ujenzi wa kuta kwenye Pwani ya Bahari ya
Hindi.
Makabidhiano
ya mtambo huu ni sehemu ya mpango endelevu wa benki wa kununua na
kukodisha mitambo (lease finance), ambayo inawawezesha wateja kujiongeza
kiutendaji kwa kupata vifaa vya kisasa bila ya kulazimika kuwa na pesa
taslimu za manunuzi ya vifaa hivyo.
Makubaliano
haya ya ukodishaji wa mitambo yanaakisi katika sekta mbalimbali ikiwemo
ujenzi, usafirishaji, teknolojia ya habari na mawasiliano, utalii,
madini, mafuta na gesi.
BANK
OF AFRICA imebaini huu ni mpango ambao una tija kubwa kwa wajasiriamali
wakubwa kwa wadogo, kwa ajili ya kufanikisha uendeshaji wa biashara zao
ambao utaongeza uzalishaji na faida kubwa. Mteja kupitia mpango huu
anapewa fursa pana ya kufanya chaguo lake bila kikwazo chochote na bila
ya uhitaji wa amana ya awali au dhamana nyingine. Marejesho ni malipo ya
ukodishaji ya kila mwezi na mteja ana uwezo wa kuchagua kua mmiliki wa
mali husika pindi ifikapo mwisho wa mkataba wa ukodishaji.
Benki
humsaidia mteja kuhakiki chombo anachotaka kuingianacho mkataba kama
kina ubora ili kuweza kuinua uchumi wake na uchumi wataifa kwa ujumla.
BANK
OF AFRICA ilianza shughuli zake Juni mwaka 2007, baada ya kuinunua
Benki ya Euroafrican ambayo ilianza kazi Tanzania kutokea September
1995.
BANK
OF AFRICA inafanya kazi katika mtandao wa benki za biashara katika nchi
18 zikiwamo nchi za Benin, Burkina Faso, Burundi, Cote d”ivoire,
Djibouti, DRC, Ethiopia, France, Ghana, Kenya, Madagascar, Mali, Niger,
Rwanda, Senegal, Tanzania, Togo na Uganda.
Kundi
la Group BANK OF AFRICA lina makao makuu yake jijini Dakar, Senegal
ikiwa na mtandao wa watu 500 wale wanaotoa huduma na sapoti kwa ofisi.
Kuanzia mwaka 2010, Group BANK OF AFRICA ilimilikiwa kwa wingi wa hisa
BMCE Bank, ambayo ni benki ya pili kwa ukubwa nchini Morocco.
BMCE
Bank huleta mikakati mizito ya msaada wa uendeshaji katika kuunga mkono
shughuli za BANK OF AFRICA Group, vilevile na muunganiko na ukaribu wa
kufikia masoko ya kimataifa kutokana na uwepo wake katika nchi za Ulaya
na Asia.
SHARE
No comments:
Post a Comment