TRA

TRA

Wednesday, July 19, 2017

MAJIMAREFU YUPO KIKAZI ZAIDI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !







Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Steven Ngonyani maarufu kama Prof Maji Marefu akitoa msaada wa kuwaokoa wananchi wa jimbo lake wakati wa mafuriko yaliyotokana na mvua miezi michache iliyopita.

UKITEMBELEA Jimbo la Korogwe Vijijini linaloongozwa na Stephen Ngonyani (CCM) maarufu kama Profesa Majimarefu utaona jinsi kuna mabadiliko makubwa ya kimaendeleo.

Mbunge huyo hayupo tayari kuona wananchi wa jimbo lake wanapata matatizo ndiyo maana anatumia kila linalowezekana kutatua kero zao. 

Kwa mfano, mwaka jana alitoa madawati 200 na kupokelewa na Mkuu wa Wlaya ya Korogwe, Robert Gabriel.


Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini (CCM) Steven Ngony'ani maarufu Proffesa Maji Marefu kulia kushoto ni Diwani wa Kata ya Kerenge wilayani Korogwe wakiwa wamebeba moja kati ya madawati 200 ambayo yalikabidhiwa na mbunge huyo kupitia Fedha za mfuko wa Jimbo kwa ajili ya shule za msingi wilayani Korogwe.
 
Hii yote ni kuhakikisha anaharakisha maendeleo ya wananchi wa jimbo hilo kwa kila mwanafunzi kusoma kwa utulivu.

Si tu kusoma kwa utulivu, lakini pia kukabiliana na tatizo hilo na kuhakikisha linaondoka. Hili nalo limefanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Jitihada za aina hiyo amezifanya maeneo mengine mengi ndani ya jimbo lake, ikiwemo sekta za afya, elimu, miundombinu, maji na wakati mwingine kutolea yeye mwenyewe ili kuhakikisha masuala ya jimbo lake hayabaki nyuma.

Hata hivyo, tukio ambalo alilifanya na kuendelea kugonga vichwa vya wananchi wengi ni pale alipojitokeza kuokoa baadhi yao wakati mvua kubwa iliponyesha.

Mbunge huyo alishiriki kwa kuwabeba na kuhakikisha anaonesha mfano badala ya kukaa na kuagiza.

Huyo ndiye Profesa Majimarefu ambaye anatumia nafasi yake kuhudumia wananchi kwa ukaribu ikiwa ni sehemu ya kutimiza wajibu wake kama mwakilishi wa wapigakura wa Jimbo la Korogwe Vijijini.


Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger