TRA

TRA

Tuesday, July 18, 2017

MDAHALO WAGOMBEA WENZA URAIS KENYA KAA LA MOTO

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
 
Utata umegubika mdahalo wa moja kwa moja ambao unafaa kuwashirikisha wagombea wenza wa urais nchini Kenya.

Mdahalo huo, ambao ungepeperushwa kupitia runinga, ulipangiwa kufanyika leo jioni, awamu ya kwanza ikishirikisha wagombea sita na ya pili wagombea wawili.

Maandalizi ya mdahalo huo yanaendelea katika Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki cha Afrika Mashariki (CUEA).

Katika awamu ya kwanza, ni mgombea mmoja pekee aliyejitokeza, Eliud Muthiora Kariara ambaye ni mgombea mwenza wa Japheth Kaluyu.

Baadhi ya wagombea wenza wa urais walikuwa wametangaza kwamba hawatashiriki katika mdahalo huo ambao ulifanyika katika Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki cha Afrika Mashariki (CUEA).

Hatua ya wagombea kutojitokeza imeonekana kuwakera baadhi ya Wakenya mtandaoni, mfano Edwin Bakanja aliyeandika: "Ukikosa kufika kwa mahojiano, usisubiri upewe kazi."

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger