TRA

TRA

Monday, July 24, 2017

RAIS MAGUFULI AWAPA TAADHARI VIONGOZI

Share On Facebook ! Tweet This ! Share On Google Plus ! Pin It ! Share On Tumblr ! Share On Reddit ! Share On Linkedin ! Share On StumbleUpon !
Rais Magufuli jana  Julai  24, 2017 ameweka jiwe la msingi katika miradi mikubwa miwili; mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria hadi Tabora, Igunga na Nzega pamoja na mradi wa ukarabati na upanuzi wa Uwanja wa ndege wa Tabora na kufungua barabara mbili za Tabora – Nyahua na Tabora – Puge – Nzega.Niwaombe viongozi Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi musimamie kero za Wananchi. 
 
Muwe mnakaa angalau kwa kila wiki kila kiongozi katika mahali alipo wasimamie matatizo ya wananchi. Matatizo ya Wananchi ni mengi wanashindwa kuvumilia wanaona Rais pekee ndiye anaweza akatatua yale matatizo. 
 
Niwaombe sana kuanzia Mkuu wa Mkoa, Mawaziri, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi muwe mnashughulikia matatizo na kuyamaliza.
 
“Nitakuwa natembelea mikoani nitakapokuwa napewa matatizo na matatizo hayo yawe yalikuwa chini ya uwezo wa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi, Katibu Tarafa, Mwenyekiti wa Kijiji kuyatatua na hakutatua, mimi nalala mbele na huyo kiongozi.” – Rais Magufuli.

Author:

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment

 
Copyright ©2016 NCHI YANGU • All Rights Reserved.
Template Design by AT Creatives • Powered by Blogger