Rais Alassane Outtara wa Côte d'Ivoire amewabadilisha
mawaziri wake wa ulinzi, bajeti na mambo ya ndani alipolivunja baraza
lake la mawaziri.
Nchi hiyo inayozalisha kakao kwa wingi zaidi ulimwenguni imejikuta
mwaka huu ikisumbuliwa na uasi wa mara kwa mara wa wanajeshi, matukio
yaliyogharimu mamia kwa mamilioni ya fedha walizobidi kulipwa wanajeshi
hao na kwa namna hiyo kuchafua sifa ya Côte d'Ivoire ya baada ya vita
vya wenyewe kwa wenyewe.Hamed Bakayoko, mtu wa karibu sana na rais Ouattara, aliyekuwa hapo awali waziri wa mambo ya ndani amekabidhiwa wizara ya ulinzi, kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa na katibu mkuu wa ofisi ya rais Patrick Achi mbele ya maripota, kabla ya mkutano wa baraza la mawaziri.
Wakati huo huo Sidiki Diakite aliyekuwa hadi sasa meya wa jiji la Abidjan ameteuliwa kuwa waziri wa mambo ya ndani.
Waziri mkuu Amadou Gon Goulibaly atakabidhiwa wizara ya bajeti akisaidiwa na Moussa Sanoogo kama katibu wa dola. Waziri wa zamani wa bajeti Abdourahmane Cisse ameteuliwa kuwa mshauri maalumu wa rais Ouattara.
Mapigano ya mwishoni mwa wiki ndio chanzo cha kuvunjwa baraza la mawaziri
Waziri wa zamani wa ulinzi Alain-Richard Donwahi amekabidhiwa hivi sasa wizara ya maji na misitu.
Itafaa kusema kwamba wanajeshi watatu waliuliwa usiku wa Ijumaa kuamkia Jumamosi iliyopita risasi zilipofyetuliwa katika kambi ya kijeshi ya Korhogo, kaskazini mwa Côte d'Ivoire. Duru za karibu na jeshi zinasema tukio hilo lilikuwa jibu kwa uasi wa kijeshi ulioigubika nchi hiyo miezi ya January na Mei mwaka huu."Maluteni wa kijeshi ndio waliokuwa chanzo cha kisa hicho lakini hadi wakati huu sababu haijulikani" duru hizo za kijeshi zimeeleza.
Mwezi january na mai mwaka huu waasi wa zamani waliojumuishwa jeshini walifanya uasi, lakini walisitisha uasi wao walipolipwa kila mmoja Euro 18.000. Kwa jumla walikuwa wanajeshi 8400. Mzozo huo uliidhofisha mno serikali ya Côte d'Ioire na hasa rais wake Alassane Ouattara ambae sifa zake zimeanza kuingia dowa.
SHARE
No comments:
Post a Comment