Meneja
Elimu kwa Mlipa kodi wa Mamlaka ya mapato Nchini (TRA), Dayana
Masala ameongoza operesheni ya kuwakamata wafanyabiashara wa vituo vya
mafuta wanaohudumia pasipo kutoa risiti na kusababishia serikali
kutokusanya mapato stahiki kwa huduma wanazotoa jijini Dar es
Salaam.
Operesheni
hiyo ilifanyika mapema jijini humo na baadhi ya vituo vya mafuta
kubambwa baadhi ya watoa huduma ya uuzaji wa nishati ya petroli na
diseli wakitoa huduma ya kwa vyombo vya moto bila kutoa risiti kwa
wateja jambo ambalo ni kinyume cha sheria za nchi jambo linalosababishia
serikali kupoteza mapato.
Bi
Msala amewaonya wafanyabiashara wenye tabia ya kutopenda kuwapa wateja
risiti kwani kwa kufanya hivyo watalazimika watakapobainika watalipa
faini ya shilingi milioni nne na nusu.
Pia
amewasisitiza wananchi kudai risiti wanapopata huduma za bidhaa
mbalimbali kwani kwa kutokufanya hivyo pia ni kosa na wakikutwa
wamenunua bidhaa bila kudai risiti watalazimika kulipa fidia ya shilingi
milioni moja na nusu.
SHARE
No comments:
Post a Comment